Thursday, February 26, 2009

Fedha za rais wa Gabon zafilisiwa nchini Ufaransa.

Fedha za rais wa Gabon zafilisiwa nchini Ufaransa.

Paris,Ufaransa - 27/02/09. Uongozi wa serikali ya Ufaransa, umefirisi fedha za rais wa Gabon, Omar Bongo Ondimba,
Uamuzi wa kufirisi fedha zake umekuja baada ya koti iliyopo Bordeaux kutoa uamuzi wa kutaka rais, Omar Bongo, kulipa fedha zilizo ingia kwenye akaunti yake, ili mfanya biashara wa Kifaransa, Rene Cardona aachiliwe kutoka jela.
Pesa zipatazo Us-$580,000, zilitolewa na mtoto wa mfanya biashara huyo, ili babayake aachiwe kutoka jela.
lakini hata hivyo koti, iliamua ya kuwa fedha hizo zilitolewa kinyume cha sheria, na kuamuliwa zirudishwe mara moja.
Picha hapo juu anaonekana rais, wa Gaboni, Omar Bongo Ondimba, akicheza muziki kusherekea miaka 70, tangu kuzaliwa kweke.
Picha ya pili anaonekana,rais, Omar Bongo, alipo kuwa moja ya mikutano ya kimataifa hivi karibuni.
Syria na Amerika kuanza mazungumzo hivi karibuni.
Washington, Amerika 27/02/09 - Ofisi ya Syria kwenye umoja wa Mataifa, imesema yakuwa serikali ya Amerika na Syria zitaanza mazungumzo hivi karibuni ili kujadiri hali ilivyo mashariki ya Kati.
Mazungumzo hayo yata wakutanisha balozi wa Syria wa nchini Amerika na viongozi wa Amerika wanaoshughulikia maswala ya mashariki ya Kati.
Katika mkutano hu watazungumzia swala la amani na hali halisi ya Mashariki ya kati kwa ujumla.
Picha hapo juu inaonekana bendera ya nchi ya Syria, nchi ambayo imekuwa inalaumiwa na Amerika kwa kujihusisha na kuyumba kwa hali ya usalama katika eneo hilo, hasa kwa kuunga mkono makundi ya Wapalestina ya nayo pingana wa Waizrael.
Picha ya pili, ni ya bendera ya Amerika, nchi ambayo imekuwa haina uhusiano mzuri na nchi ya Syiria.
CIA yasema Kim Jongo Il, bado ashikilia uskani.
Pyongyang,Korea ya Kaskazini - 27/02/09.Shirika la Kijasusi la Amerika -CIA- limesema ya kuwa kiongozi wa Jamuhuri ya Korea ya Kaskazini,Kim Jong Il, bado anaongoza nchi, japokuwa imeripotiwa hali yake ya afya siyo nzuri.
Haya yalisemwa na Leon Panetta wakati alipo kuwa akiongea na waandishi wa habari, kuhusu nia ya Korea ya kaskazini, kutaka kurusha mizimga ya ke ya masafa marefu kwa majaribio.
Picha hapo juu anaonekana kiongozi wa Korea ya Kaskazini, Kim Jong Il,akiongea na baadhi ya viongozi wa Korea ya Kaskazini,kabla ya kuwa kwenye matibu kwa kipindi kilefu sasa.
Vyama vya Wapalestina kukubaliana kushirikiana kimsingi.
Kairo,Misri - 27/02/09. Makubaliano ya kimsingi yamefikiwa kati ya vyama pinzani vya Fatah na Hamas ambayo vinaongoza Wapalestina ili kujadili jinsi gani vinaweza shirikiana.
Baada ya mkutano huo uliofanyika Misri, mmoja ya kiongozi wa Fatah,Ahamed Qurei, alisema uamuzi huo ni kwa ajili ya Wapalestina wote waishio Ukanda wa Gaza na West Bank.
Hata hivyo, kiongozi huyo akuelezea kiundani zaidi nini makubaliano yapi watajadili.
Picha hapo juu, ni ngao ya bendera ya Fatah, chama ambacho kimekuwa kikipigania haki za Wapalestina tangu kianzishwe mwaka 1954.
Picha ya pili ni ya ngao ya chama cha Hamas, chama ambacho kimekuwa kikipigania Wapalestina, huku kikiwa na mwelekeo tofauti na Fatah.

No comments: