Tuesday, February 17, 2009

NATO kuangalia kwa makini makubaliano ya Taliban na Pakistan.

Venezuela wapiga kura ya maoni" Rais ataweza kutawala zaidi ya miula miwili"Wakubali wanachi wa Venezuela".

Caracas,Venezuela - 17/02/09. Wananchi wa Venezuela, wamepiga kura ya maoni kupitisha mswaada wa kumruhusu mwanachi yoyote ambaye atakuwa rais, kuweza kutawala zaidi miula miwili iliyo kuwa imewekwa hapo mwanzo katika katiba ya Venezuela.
Kura zilizo kubali mswada huo zilifikia asilimia 54, na kukubaliana na mswada huo ulio pendekezwa na rais Hugo Chavez.
Kufuatia kura hiyo rais, wa sasa wa Venezuela, Rais, Hugo Chavez ataweza kugombania tena urais pindipo kipindi chake cha urais kitakapo kwisha mwaka 2012.
Picha hapo juu anaonekna , rais Hugo Chavez, akiongea na wanchama na wanchi walio kuja kumsikiliza baada ya matokeao ya kura ya maoni.
Picha ya pili, wanaonekana melfu ya wananchi wakishangilia, baada ya ya matokeo ya kura ya maoni kutangazwa.
NATO kuangali kwa makini makubaliano ya Taliban na Pakistan.
Mingora, Pakistan - 17/02/09.Nchi wanachama wa NATO, wa wameonya kuhusu serikali ya Pakistan kuanza kuongea na kundi la Taliban.
Onyo ilimekuja baada ya serikali ya Pakistan, kukubali kuwepo kwa sheria za kidini katika jimbo la Swat.
Kwa mujibu wa NATO, wanaangali kwa makini sana hali hii.
NATO ambayo inawanajeshi zaidi ya 55,000 katika maeneo tofauti kati ya mipaka ya Afghanistan na Pakistani katika vita vya kupambana na ugaidi.
Picha hapo juu ni bendera ya NATO na bendera zanchi wanchama wake.
Iran na Urusi zafanya mazungumzo ya ushirikiano wa kijeshi.
Teheran,Iran - 17/02/09.Serikali ya Iran inafanya mazungumzo na serikali ya Urusi, katika jitihada za Iran kuweza kushirikiana na Urusi katika nyanja za kijeshi
Mazungumzo hayo yaliyo wakutanisha waziri wa ulinzi wa Urusi, Anatoly Serdyukov na waziri wa ulinzi wa Iran, Mostaf Najar, yalilenga hasa ji jinsi gani serikali ya Irani itaweza kupata mizinga ya kijeshi ya kuzuia ushambuli wa anga.
Picha hapo juu ni picha ya ya moja ya mitambo ya kijeshi ya Iran,ambayo ipo kwa ajili ya kuzuia mashambulizi ya anga.
Serikali ya Amerika yaionya Korea ya kaskazini.
Tokyo,Japan - 17/02/09. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Bi, Hillary Clinton ameionya serikali ya Korea ya Kaskazini, ya kwamba mpango wake wa kutaka kujaribu kurusha mabomu ya nyukili kitakuwa ni kitendo ambacho jumuia ya kimataifa haitakikubali.
Bi, Hillary Clinton,aliyaongea haya wakati alipo kutana na viongozi wa serikali ya Japan, ambapo yupo ziarani nchini humo Japan.
Picha ya hapo juu anaonekana , Bi Hillary Clinton,akisalimiana na waziri wa mabo ya nchi za nje wa Japan Hirofumi Nakasone,mapema walipo kutana mjini Tokyo.

No comments: