Thursday, February 19, 2009

Rais, Baraka Obama, afanya ziara yake ya kwanza nje ya Amerika tangu kuapishwa kuwa rais wa Amerika.

Hakuna amani mpaka askari wetu aachiliwe huru"Serikali ya Izrael ya dai"

Cairo, Misri - 19/02/09. Makataba wa makubaliano wa kuleta amani katika ukanda wa Gaza,umeingia katika hatua nyingine ya utata.
Habari kutoka katika serikali ya Misri, zimesema, jambo la serikali ya Izrael kusema ya kuwa, ili pawepo na amani, ni lazima askari wa Izrael aliye kamatwa mwaka 2006, aachiwe huru na kundi la hamas, litaleta ugumu wa kuwepo na amani ya kudumu katika maeneo ya Ukanda wa Gaza. Kwa mujibu wa habari hizo zina sema, katika mkataba huo hakukua na makubaliano au maelezo ya aina yoyote yanayo husu kuachiwa kwa askari huyo ndipo kutaleta amani katika eneo hilo la Ukanda wa Gaza.
Askari huyo, Gilad Shalit aliyekamatwa mwaka 2006 mwezi wasita karibu na mpaka wa Gaza.
Picha hapo juu ni Izrael, nchi ambayo imekuwa na wakati mgumu hasa kwa wanasiasa, ni njia gani watatumia kumpata askari Gilad Shalit, kutoka mikononi mwa kundi la Hamas.
Picha ya pili, ni ya moja ya bendera ya Hamas,kundi ambalo limekuwa likimshikilia askari Gilad Shalit tangu mwaka 2006.
Picha ya chini ni ya nchi ya Misri,nchi ambayo imekuwa ikijitahidi kuleta maelewano na mapatano kati ya Izrael na kundi la Hamas na uongozi wa Wapalestina kwa jumla.
Rais, Baraka Obama, afanya ziara yake ya kwanza nje ya Amerika tangu kuapishwa kuwa rais wa Amerika.
Ottawa, Kanada-19/02/09. Rais wa Maerika, Baraka Omaba, amefanya ziara ya kwanza ya kimataifa nchini Kanada tangu ahapishwe kuwa rais wa Amerika.
Rais, Obama, katika ziara hiyo, anatarajiwa kuzungumzia kiundani zaidi ushirikiano wa karibu wa nchi hizi mbili na na wenyeji wake viongozi wa Kanada.
Picha hapo juu, wanaonekna baadhi ya watu, wakiwa wamebeba mabango ya kumkaribisha rais wa Amerika, Baraka Obama, nchini Kanada ikiwa ndiyo ziara yake ya kwanza ya kiserikali tangu awe rais wa Amerika.
Picha ya pili, anaonekna rais wa Amerika ,Baraka Obama, akipewa saruti na mmoja ya wanajeshi wa Kanada, wakati alipo wasili kwenye uwanja wa ndege.
Picha ya tatu, wanaonekana, rais wa Amerika , Baraka Omaba, na mwenyeji wake,Mkuu wa jimbo la Ottawa,Michelle Jean, wakikagua gwaride la heshi lililo andaliwa na kwa ajili ya rais Baraka Obama.
Muungano wa Ulaya wakosolewa na rais wa Czech.
Brussel, Belgium-19/02/09.Rais wa Czech, Vaclav Klaus,amekosoa utendaji wa Muungana wa nchi za Ulaya kwa kufanya baadhi ya kazi ambazo zinaenda kinyume na Muungano huo.
Huku akishangiliwa na baadhi ya wabunge na wengine kutoka nje, rais Vaclav Klaus, alisema yakuwa umoja huo umekuwa na muundo ambao hautoi nafasi zaidi, kwani wale wanaotoa mawazo yao tofauti wamekuwa wakiitwa wana pinga Muungano wa Ulaya.
Picha hapo juu, anaonekna rai wa Czech, akinyoosha kidole kusisitizia nini anamaaanisha, wakati alipo hutubiwa bunge la Muungano wa nchi za Ulaya.
Bunge lapiga kura, kufunga kambi ya jeshi inayo tumiwa na Amerika.
Manas,Kirgizstan-19/02/09.Bunge la Kirgizstan limepiga kura kwa wingi kufunga kambi na uwanja wa ndege uliopo nchini humo kwa matumizi ya jeshi la Amerika.
Katika kura hizo zilizo pigwa,kura zilizo kubali kufungwa kwa kambi na kiwanja hicho cha ndege zilikuwa 78 na zilizo kataa kufungwa kwa kiwanja hicho ni kura 1.
Kambi hiyo iliyo kuwa muhimu kwa jeshi la Amerika katika kuendeleza vita vyake nchini Afghanistan,imetakiwa kufungwa kwa kipindi kisicho pungua miezi sita.
Picha hapo juu zina onekana ndege za kijeshi za Amerika, zikiwa zimesimama kwenye uwanja huo uliopo Manas na ndege nyingine inaonekna ikikaribia kutua uwanjani.
Picha ya tatu, anaonekana mmoja ya wanajeshi wa Amerika, akiwa amebeba zana zake, na miezi michache hatakuwa tena katika eneo la Manas kama kambi yake (yao) ya kijeshi.

No comments: