Friday, February 20, 2009

Kesi ya aliyemrushia kiatu aliyekuwa rais wa Amerika ya hairishwa.

Papa wapunguza mashambulizi kwa binadamu"Wasema wataalaamu".

Frolida, Amerika - 20/02/09.Wataalamu wa tabia ya viumbe viishivyo baharini ,wamesema mashambuli ya papa kwa binadadmu yamepungua kwa kiasi kikubwa katika mwaka 2008kwa kulinganisha miaka mitano iliyo pita.
Akiongea hayo, mwanasayansi anayeshughulikia tabia za papa, alisema mwaka 2008, papa walipunguza mashambuli kwa binadamu,kwani ni watu wawili walipoteza maisha kutokana na kujeruhiwa na papa, nchini Mexico, Amerika mmoja na Australia mmoja.
Picha hapo juu anaonekana papa, akiwa amemza binadamu maara baada ya kushambulia.
Picha ya pili, anaonekna papa, akiluka juu ya maji tayari kushambua kitu chochote anacho hisi kipo mbele yake.
Kesi ya aliye mrushia kiatu aliyekuwa rais wa Amerika ya hairishwa.
Baghdad,Irak-20/02/09. Wanachi wa Irak, wamshuhudia Muntedar al Zaidi mwenye miaka 30, akifikishwa mahakamani kwa kosa la kumtupia kiatu aliyekuwa rais wa Amerika, George Bush, wakati alipo fanya ziara nchini Irak, kabla ya muda wake wa kuwa rais wa Amerika kuisha.
Muntader al Zaidi, alifika mahakamani, hasubuhi ya siku ya alkhamis 19/02/09, huku akishuhudiwa na ndugu ,jamaa, marafiki, wanasheria, wanasiasa na wanchi wengine.
Katika kesi hiyo,watu walisikika wakipiga kelele, ambazo zilimpa wakati mgumu hakimu na kuchukua muda zaidi ya saa na dakika 15.
Hata hivyo, hakimu alihairisha kesi hadi 12/machi/2009
Zimbabwe yaitaji billion 5$- dola,"Asema waziri mkuu"
Harare,Zimbabwe - 20/02/09. Waziri mkuu mpya wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai, amesema,ili kujenga na kunyanyua uchumi wa Zimbabwe,kunaitajika zaidi ya billion 5$ - dola.
Na hii inaitakuja kutoka na vitega uchumi vitakavyo wekwa na wawekezaji.
Waziri mkuu, huyo wa Zimbabwe, aliyasema haya wakati alipo kuwa baada ya kukutana na rais wa Afrika ya Kusini na waziri wa fedha,ili kujadili ni njia zipi zita tumika kusaidia kunyanyua haraka uchumi wa Zimbabwe.
Picha hapo juu ni ya bendera ya Zimbabwe, nchi ambayo imekuwa katika hali mbaya ya kiuchumi tangu kuanza matatizo ya kisiasa,baada ya uchaguzi mkuu wa uliofanyka mapema mwaka 2008.
Picha ya pili anaonekana waziri mkuu wa Zimbabwe, Morgan Tsvangirai, akiongea huku akiangali kwenya faili lake lililo juu ya kijukwaa, nakujaribu kuafafanua kwa undani, huku akionyesha mikono juu, kuashiria hali ya uchumi ya Zimbabwe, inahitaji kujengwa upya.
Kiongozi wa Likud, Benjamin, Netanyahu, atakiwa kuunga serikali.
Jerusalem, Izrael- 20/02/09 - Rai wa Izrael, Shimon Peres, amembomba kiongozi wa chama cha Likud, Benjamin Netanyahu kuunga serikali ya muungano kwa muda usiopungua wiki sita.
Rais, Shimon Peres, alimuomba, bwana Benjamin Netanyahu, wakati walipo kutana, na baadaye kuongea katika mkutano uliofanyika Jerusalem.
Katika, mkutano huo, bwana, Benjamini Netanyahu, aliwaomba viongozi wa vyama pinzani kuungana kwa pamoja, ili kuweza kuunda serikali kwa ajili ya wana nchi Izrael.
Picha ya hapo juu wanaonekana, rais, Shimon Peres na kiongozi wa chama cha Likud, bwana Benjamin Netanyahu, wakisalimiana muda mfupi kabla ya kuanza mazungumzo.
Picha ya pili, anaonekana, kiongozi wa chama cha Likud, Benjamin Netanyahu, akiongea kwa kusisitiza lazima waungane ili kujenga Izrael.
Tamil Tager washambulia ndani ya jiji la Kolombo"Hali si swali Sri Lanka"
Kolombo, Sri Lanka - 20/02/09. Watu wapatao 50 wamjeruhiwa vibaya na wengine wawili kuuwawa baada ya ndege za kijeshi la kundi la Timil Tiger, kushambulia ndani ya jiji la Kolombo.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Sri Lanka,Kaheliy Rambukwella, alisema yakuwa ndege hizo zilishambulia majengo ya serikali.
Hata hivyo moja ya ndege hizo za kijeshi, ilishambuliwa na ndege za jeshi la serikali.
Mapambano kati ya jeshi la serikali na kundi la Tamil Tiger ambalo linagombani kujitenga na serikali.
Picha hapo juu, zinaonekna gari zikiendeshwa kwa kasi ili kuepuka milipuko, mara ya milipuko kusikika karibu na mojo ya majengo yenye ofisi za serikali.
Picha ya pili ni ramani ya Sri Lanka, nchi amboyo imekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, tangu mwazo wa mwaka 1983.

No comments: