Monday, May 10, 2010

Gordon Brown asema "Nangátuka madarakan."

Gordon Brown asema "Nangátuka madarakani."

London,Uingereza - 10/05/2010. Waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown amesema atajiudhuru uongozi katika chama chake cha Labour, na kuwaomba wanachama wenzake kujiandaa kumchagua kiongozi mwingine atakaye kiongoza chama cha Labour.
Akiongea mbele ya wandishi wa habari Gordon Brown alisema "nita jiudhuru uongozi wa chama ifikapo wa mwezi Septemba" Na kwa sasa kiongozi wa Liberal Demokratic, Nick Clegg,ameniambia ya kuwa angetaka kuongea na chama cha Labour wakati anaendelea kujadiliana na chama cham Consevative."
Akimalizi katika hotuba yake Brown alisema "Katika kipindi chote nitakacho kuwa kiongozi kabla ya kujiudhulu nitahakikisha mabadiliko ya kiuchumi yanakwenda haraka na kukamilisha yale yote yanayotakiwa kufanywa kwa maendeleo ya Waingereza wote."
Picha hapo juu anaonekana waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown akiongea mbele ya waandishi wa habari mikakati na muda gani atajiudhulu uongozi.

No comments: