Friday, May 7, 2010

Uchaguzi wa Uingereza wawa patupu.

Uchaguzi wa Uingereza wawa patupu. London Uingereza - 07/05/2010. Matokeo ya uchaguzi yaliyotolewa nchini Uingereza yameiacha nchii hiyo na wakati mgumu wa kisiasa baada ya matokeo hayo kutompa mgombea yoyote wa vyama vya, Conservatives, Labour na Liberal Demokrati ushindi kamili wa kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo. Matokeo hayo ambayo Conservatives ilipata viti 306 au asilimia 36%, Labour viti 258 asilimia 29% na Liberal demokrati 23%. Kufuatia matokeo hayo ya uchaguzi, serikali ya Uingereza itabidi iundwe na chama zaidi ya kimoja tangu hali hii ilipo tokea mwaka 1974. Picha hapo juu wanaonekana wagombea wa uongozi wa Uingereza wakati wa kampeni ya uchaguzi hivi karibuni, kutoka kushoto, David Cameroon, Nick Clegg na Gordon Brown. Taliban na Al Qaeda washirikiana zaidi.

Islamabad, Pakistan - 07/05/2010. Habari kutoka katika ofisi kuu za kijasusi za kimataifa zinasema yakuwa "kundi la Taliban na Al Qaeda zimekuwa na huusiano wa karibu zaidi kuliko hapo mwanzo na kuongea hali ya usamala kuwa wa mashaka kwa wanchi wa Afghanistan na nchi zinazo pakana na nchi hiyo."
Wachunguzi wa mambo ya kijasusi walizidi kusisitiza habari hizi hasa kwa kuzingatia uwezo wa mwanzo wa kundi la Taliban.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya wapiganajiwa kundi la Taliban ambao wamekuwa wanapigana na majeshi ya kimataifa nchini Afghanistan.

No comments: