Thursday, May 6, 2010

Nigeria yapata msiba mkubwa.

Nigeria yapata msiba mkubwa.

Lagos, Nigeria 06/05/2010. Aliyekuwa rais wa Nigeria,Umuru Yar'Adua amefariki dunia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Marehemu, Umuru Yar'Dua alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa na hata aliweza kwenda nchi za Kiaarabu kwaajili ya matibabu zaidi na baadaye aliweza kurudi nchi Nigeria mapema mwezi wa Februari.
Kufuatia kifo hicho, aliyekuwa makamu wa rais Jonathan Goodluck ameapishwa kuwa rais wa Nigeria baada ya kifo cha aliyekuwa rais umuru Yar'Dua. Picha hapo juu anaonekana hayati raia wa Nigeria, Umuru Yar'Dua enzi za uahai wake akiongea katika mkutano mmoja wapo.
Picha ya pili wanaonekana wanajeshi wa Nigeria, wakiwa wamebeba mwili wa marehemu rais wa Nigeria Umuru Yar'Dua kuelekea kijijini kwa ambapo alipewa pumuziko la milele mbele ya familia, ndugu,wananchi na raia wa sasa Goodluck Jonathan.
Picha ya tatu anaonekana akiapa kuwa rais wa Nigeria baada ya kutangazwa ya kuwa rais Umuru Yar'Dua amefariki dunia.
Jeshi la Urussi laokoa meli ya iliyotekwa nyara.
Moscow, Urussi - 06/05/2010. Jeshi la wanamaji la Urussi limeikomboa meli iliyo kuwa imetekwa na maharamia wa Kisomalia siku chache zilizo pita katika maeneo ya bahari ya Ghuba ya Uajemi.
Kwa mujibu wa msemaji wa jeshi alisema "Katika harakati za kutaka kuikomboa meli hiyo maharamia 10 walifariki dunia na wengine walikamatwa."
Meli hiyo ambayo ilikuwa inawafanyakazi wapatao 23 ambapo meli hiyo ilikuwa imebeba mafuta yenye thamani ya $52 million kuelekea nchini China.
Picha hapo juu wanaonekana baadhi ya maharamia wa Kisomalia wakiwa katika ufukwe wa wa pwani ya Somali.

No comments: