Friday, May 14, 2010

Swala la mto Nile lafikiwa muafaka na nchi nne.

Swala la mto Nile lafikiwa muafaka na nchi nne.

Kampala, Uganda - 14/05/2010. Serikali za nchi za Rwanda, Uganda, Ethiopia naTanzania zimetialiana sahii mkataba ili kuanza kuangalia ni kwa jinsi gani nchini hizi zitaanza kufaidika na malia asili ya mto Nile kwa manufaa ya nchi hizo na kutengua mkataba uliwekwa na ukoloni wa Uingereza mwaka 1929 ambapo Misri ilipewa haki ya kutumia maji ya mto huo kwa wingi kuliko nchi zote ambazo mto huo unatoka au kupita.
Wakiongea kwa nyakati tofauti mawaziri wa maliasili wa Ethiopia Asfaw Dingamo alisema " naamini hatimayake nchi zpte zitakubaliana kimsingi kuhusu swala zima la matumizi maji ya mto Nile."
Naye waziri wa maliasi wa Rwanda, Stansilas Kamanzi alisema " inasikitisha baadhi ya nchi ambazo mto una pita hazikuwepo kutokana na hali halisi ya swala lenyewe."
Kufuatia kitendo hicho, serikali ya Misriimepinga na kudai haikuwa haki na huenda ikachukua hatua za kisheria.
Picha hapo juu inaonyesha vyanzo vya mto Nile kutoka Afrika ya mashariki na kuishia nchini Misri.
Picha ya pili inaonyesha picha ya maji ya mto Nile ambayo yamekuwa yakitumiwa kwa njia mbalimbali na wanchi wa Misri kwa asilimia kubwa.
Rais wa Urussi akutana na kiongozi wa Hamas.
Dumuscas,Syria - 14/05/2010. Rais wa Urussi, Dmitry Medvedev amekutana na kiongozi wa kundi la Hamas aliyepo ukimbizini nchini Syria Khaled Meshaal wakati wa ziara yake aliyo ifanyanchini humo.
Kufuatia mkutano huo, ofisi za mambo ya nje ya Izrael zimesema"hazikufurahishwa na kitendo hicho."
Hata hivyo habari kutoka ofosi za serikali ya Urussi zinasema" kiongozi huyo huwa nakutana au kuwasialiana viongozi wengi wakiwemo wa serikali ya Amerika ila kutokana na sababu fulani huwa hawatangazwi kama walikutana au kuwasiliana na kiongozi huyo."
Picha hpo juu ni ya rais wa Urussi, Dmitry Medvedev, ambaye alikutana na kiongozi wa kundi la Hamas aliyepo ukimbizini nchini Syria.
Rais Obama, ataka muswada wa kutengenezwa mitambo ya ulinzi upitishwe.
Washington, Amerika - 14/05/2010. Rais wa Amerika Baraka Obama, amelitaka bunge la Congress kupitisha muswada wa pesa $205million kwa ajili ya kuisaidia Izrael kutengeneza mitambo ya kuzuia mashabulizi ya mabomu.
Mpango huo unao julikana kama "Iron Dome" utakuwa na mazumuni ya kuzuia mashambulizi kutokea nchini za jirani hasa Lebanon na Ukanda wa Gaza ambapo huwa mabomu mengi huwa yanarushwa upande wa Izrael kutokea sehemu hizo.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Amerika, Baraka Obama akiongea hivi karibuni kuhusu hali halisi ya Mashariki ya Kati.
Taliban wataka utawala wa Pakistan ung'olewe.
Karachi, Pakistan - 14/05/2010.Kiongozi mmoja wa kundi la Taliban liloponchini Pakistan Azam Tarik amelitaka kundi lake kuingusha serikali ya Pakistan na kusema ya kuwa nia na mipango ya Amerika haitafanikiwa.
Kiongozi huyo ambaye pia ni msemaji wa kundi hilo alisema "kundi lake halijahusika na milipuko ya mabomu iliyo tokea hivi karibuni katika maeneo yanayo kaliwa na raia, na ni mbinu za kutaka kulichafua kundi hilo."
Akisisitiza Azam Tarik, "hivi sasa umefika wakati wa kuwaondowa kwenye madaraka wale wote wanao shirikiana katika kupinga Uislaam na wananchi wa Pakistan."alimalizia kwa kusema.
Picha hapo juu anaonekana rais wa Pakistan, Asif A Zardari, ambaye yupo madaraka na hali ya usalama wa Pakistani imekuwa nawakati mgumu kutona na tishio la kundi la Taliban.

No comments: