Wednesday, May 12, 2010

Uingereza yapata serikali mpya ya shirikisho.

Uingereza yapata serikali mpya ya shirikisho.

London, Uingereza - 12/05/2010. Wananchi wa Uingereza wamepata viongozi wapya watakao iongoza serikali ya nchi hiyo baada ya makubaliano ya kimsingi kufikiwa kati ya chama cha Liberal Demokratik na Conservative.
Serikali hiyo mpya shirikisho itaongozwa na waziri mkuu mpya wa Uingereza David Cameron wa chama cha Conservative na makamu wa waziri mkuu atakuwa Nick Gregg wa chama cha Liberal Demokratik.
Picha hapo juu wanaonekana viongozi wapya wa serikali ya Uingereza, David Cameron kushoto akiwa na Nick Gregg kulia wakielekea kuingia ofisini kuanza kazi ya uongozi rasmi.
Picha ya pili, wanaonekana Nick Cregg kulia na David Cameron kushoto wakiwasalimia wananchi na waandishi wa habara mara baada ya kukubaliana kimsingi kuunda serikali ya shirikisho ya Uingereza.
David Miliband atangaza kugombea uongozi wa chama cha Labour.
London, Uingereza - 12/05/2010. Aliyekuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza David Miliband ametangaza kugombe kiti cha uenyekiti cha cham cha Labour.
David Miliband ambaye ameshawahi kushika madaraka tofauti katika serikali iliyokuwa ikiongozwa na chama cha Labour kabla ya kuteuliwa kuwa waziri wa mabo ya nje wa Uingereza.
Picha hapo juu anaonekana David Miliband ambaye ametangaza kugombea uongozi wa chama cha Labour.
Picha ya pili anaonekana aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown akishuka kutoka kwenye gari baada ya kutoka kumwona Malkia wa Uingereza ya kuwa anaikabidhi serikali kwa chama cha Conservative na Libaral Demokratik.
Urusi na Uturuki kushirikiana kwa ukaribu.
Ankara, Uturuki - 12/05/2010. Serikali ya Urussi imetiliana sahii mkataba na serikali ya Uturuki wenye thamani ya $20 billion kwa ajili ya kujenga mitambo ya kinyuklia na miradi mingine.
Kwa mujibu wa wasemaji wa serikali zote mbili walisema "nchini hizo pia zimeondo visa kwa raia wa nchi hizo na kurahisisha shughuli nyingine za kujenga mahusiano kati ya nchi hizo mbili."
Picha hapo wanaonekana rais wa Urussi kulia Dmitry Medvedev na waziri mkuu wa Uturuki Tayyip Erdogon wakitia sahii mikataba kwaniaba ya nchi hizo mbili.
Ndege yaanguka na kuuwa abiria 103 nchini Libya.
Tripoli, Libya - 12/05/2010. Ngede iliyo kuwa ikitokea nchi Afria ya Kusini kuelekea nchini Libya imeanguka na kupoteza maisha ya watu 103 na kijana mmoja wa Kihollanzi ndiye aliye nusirika katika ajali hiyo.
Kwa mujibu wa habari zina sema "ndege hiyo ilianguka karibu na kiwanja cha ndege wakati inataka kutua."
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Afriqiya ilikuwa katika safari zake za kawaida kutoka jijini Johannesburg kuelekea jijini Tripoli.
Picha hapo juu yanaonekana mabaki ya ndege la Afriqiya ambayo ilianguka mapema alfajiri siku ya Jumatano ikitokea nchini Afrika ya Kusini.

No comments: