Monday, January 13, 2014

Areal Sharon alazwa nyumba yake ya milele.

Areal Sharon alazwa nyumba yake ya milele.

Tel Aviv, Izrael - 13/01/2014. Mamia ya Waizrael wameudhuria mazishi ya aliyekuwa waziri mkuu na amiri jeshi wa nchi hiyo Areal Sharon.

Mazishi ya waziri Areal Sharon yalifanyika katika shamba leke  kwenye eneo la jangwa la Negev.

Waziri mkuu wa sasa wa Izrael Benyamin Netanyahu ambaye aliongoza mazishi kwa niaba ya serikali, alisema " Sharon ni moja ya komanda wa Kiizrael ambao watakumbukwa kwa kuitete Izrael na Wajuishi "












Mazishi ya Areal Sharon yameudhuliwa na makamu wa rais wa Mareakani Joe Biden, waziri wa mambo ya nje wa Urusi, Sergi Levrov, aliyekuwa waziri mkuu wa Uingereza Tony Brair na viongozi wengi kutoka sehemu tofauti duniani kasoro viongozi kutoka Afrika na Amerika ya Kusini.

Areal Sharon 85, alifariki kutokana na kuugua kwa  baadhi ya viongo vyake vya ndani ya mwili, na hii ilitokana hapo mwanzo wa mwaka 2006 kupata ugonjwa wa kiaharusi ambao ulimsababishia kulazwa kwa muda wa miaka saba.

No comments: