FIFA ya Sepp Blatter yafanya alicho takiwa kupewa Pele.
Akiongea baada ya kupokea zawadi hiyo ya mpira wa dhahabu, ambao umeanzishwa kwa mara ya kwanza, Pele alisema "sasa naona ndoto yangu imekamilika, kwani nimekuwa na wivu kuona wengine wakitunukiwa na hivyo kwa sasa nina kombe vyote nilivyo kuwa navihitaji"
Sepp Blatter ambaye ni rais wa shirikisho la mpira wa miguu FIFA akimsifu Pele alisema" Hakuna mchezaji ambaye amemfikia Pele katika historia ya mpira wa miguu duniani.
"Amefunga magoli zaidi ya alfu moja na kuwafanya watu wapende mchezo wa mpira wa miguu pote duniani na kwa uwezo wake wakusakata soka, na ni mchezaji wa karne ya 20"
Pele hakuweza kupata zawadi hii ya mpira wa dhahabu kwa kuwa mchezaji bora wa dunia enzi za uchezaji wake, kwa sababu alikuwa hajawahi kucheza ligi za Ulaya japo alikuwa akitikisa dunia kwa umairi wake wa kusakata soka na kuwanyanyasa mabeki na makipa kugalagala na kurudi nyavuni kuotoa mpira ulio tikisa nyavu.
No comments:
Post a Comment