Monday, January 13, 2014

FIFA ya Sepp Blatter yafanya alicho takiwa kupewa Pele.

FIFA ya Sepp Blatter yafanya alicho takiwa kupewa Pele.

Zurich, Uswizi - 13/01/2014. Edson Arantes Nascimento alimaarufu kama Pele, ametunukiwa zawadi maarumu ya mpira wa dhahabu  na kutambulika kuwa yeye  ndiye alikuwa mchezaji bora wa dunia katika karne 20 na mpa sasa hakuna ambaye amamesha wahi kuvunja rekodi yake ya usakataji wa soka na ufungaji wa magoli duniani kote hadi sasa.

Akiongea baada ya kupokea zawadi hiyo ya mpira wa dhahabu, ambao umeanzishwa kwa mara ya kwanza, Pele alisema "sasa naona ndoto yangu imekamilika, kwani nimekuwa na wivu kuona wengine wakitunukiwa na hivyo kwa sasa nina kombe vyote nilivyo kuwa navihitaji"

Sepp Blatter ambaye ni rais wa shirikisho la mpira wa miguu FIFA akimsifu Pele alisema" Hakuna mchezaji ambaye amemfikia Pele katika historia ya mpira wa miguu duniani.
"Amefunga magoli zaidi ya alfu moja na kuwafanya watu wapende mchezo wa mpira wa miguu pote duniani na kwa uwezo wake wakusakata soka, na ni mchezaji wa karne ya 20"

Pele hakuweza kupata zawadi hii ya mpira wa dhahabu kwa kuwa mchezaji bora wa dunia enzi za uchezaji wake,  kwa sababu alikuwa hajawahi kucheza ligi za Ulaya japo alikuwa akitikisa dunia kwa umairi wake wa kusakata soka na kuwanyanyasa mabeki na makipa kugalagala na kurudi nyavuni kuotoa mpira ulio tikisa nyavu.


No comments: