Saturday, January 11, 2014

Waziri wa ulinzi wa Uingereza hausishwa na mateso wafungwa Irak.

Waziri wa ulinzi wa Uingereza hausishwa na mateso ya wafungwa Irak.

London, Uingereza - 11/01/2014. Shirika la kutete haki za binadamu na katiba ya Ulaya lenye makao yake nchini Ujerumani limeiomba mahakama inayoshughulikia makaosa ya jinai ICC, kuchunguza matendo ya uvunjwaji wa haki za binadamu uliofanywa na viongozi wa serikali wa Uingereza.

Likiataja shirika hilo limesema "Geoff Hoon ambaye alikuwa waziri wa ulinzi na katibu mkuu  Adam Ingram kuwa walihusika kwanjia moja au nyingine katika mateso na mantendo yaliyo kuwa yanakuiuka haki za binadamu kati ya mwaka 2003 na 2008 na kuvunja sheria ya Geneva ya kulinda wafungwa wa kivita."

Hata hivyo watu hao ambao wanashukiwa kufanya makosa hayo wamekana kuhusika na makosa hayo.

Kesi hiyo ambayo ina kurasa 250,  ilikabidhiwa kwa ICC, huku ikiwa na makosa 85 ambayo inasemekana yamevunjwa  na viongozi hao, na hivyo kuomba wachunguzwe.

Wakati wa vita vya Irak, wanajeshi wa Uingereza walishutumiwa kwa kuhusika katika kutesa wafungwa wa kivita, ambapo Geof Hoon alikuwa ndiye mkuu wa wizara ya ulinzi ya nchi ya Uingereza.





No comments: