Monday, January 13, 2014

Cristiano Ronaldo atunzwa mpira wa dhahabu kwa mara ya pili.

Cristiano Ronaldo atunzwa mpira wa dhahabu kwa mara ya pili.

Zurich, Uswizi - 13/01/2014. Mchezaji wa Real Madrid  Cristiano  Ronaldo amechaguliwa kuwa mcheaji bora wa dunia wa mwaka 2013

Cristiano Ronaldo 28, amechaguliwa  kwa kura 1,365  na kuwashinda wachezaji wenzake wawili Lionel Messi  1,205 wa timu ya Barcelona.



 Na Frank Ribery 1,127 wa Buyen Munich ambao walifikia fainali katika uchaguzi huo.

Akiongea baada ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa dunia wa mwaka 2013, Cristiano Ronaldo alisema, " sina cha kusema, na nawashukuru wachezaji wenzangu, uongozi kwa jumla, kwani kupata tunzo hili siyo rahisi."

Tuzo hili la kuwa mchezaji bora wa dunia litakuwa ni la mara ya pili katika maisha yake Cristiano Ronaldo ya kimpira kufuatia la kwanza alilopata mwaka 2008.



No comments: