Kesi ya Rafiki Hariri yaanza na kuhamishia masikio ya Walebanoni jijini Hague.
Kesi hiyo imefunguliwa dhidi ya watu nne Mustafa Badreddine, Salim Ayyash, Hussin Oneissi na Assad Sabra ambao pia inasadikiwa kuwa ni wanacham wa kundi la Hezbollah kundi ambalo linashutumiwa kuhusika katika mauji ya Rafiki Hariri.
Hata hivyo kesi hiyo imeanza huku watuhumiwa kutokuwepo mahakamani na jaji David Re kuamua kuwa kesi itaendelea kwa "watuhumiwa kukana kosa hilo."
Rafiki Hariri, na watu wengine 22 waliuwawa mwaka 2005, baada milipuko ya abomu kutoe katika eneo ambalo walikuwepo na kundi la Hezbollah kushutumiwa kuhusika na mauaji hayo, japo kundi hilo limekana kuhusika na mauaji hayo na pia kuipinga mahakama hiyo.
Hata hivyo baada ya kuuwawa kwa Hariri, jeshi la Syria lililazimika kuondoka nchini Lebanoni ambapo jeshi hilo lilikuwa likilinda amani nchi Lebanoni.
No comments:
Post a Comment