Saturday, January 11, 2014

Aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael hatupo naye tena kimwili.

Aliyekuwa waziri mkuu wa Izrael hatupo naye tena kimwili.

Tel Aviv, Izrael - 11/01/2014. Wanachi wa Izrael wamekubwa na msiba mkubwa kufutia kifo cha aliyekuwa waziri mkuu na amiri jeshi wa nchi hiyo kutokea leo hii.

Ariel Sharon 85, ambaye alikuwa amelazwa hospital kwa muda mrefu, baada ya kukumbwa na ugonjwa wa kiharusi mwaka 2006  na ambapo  ulisababisha akupata madhara ndani ya viongo vya mwili wake na kupelekea kifo.

Shlomo Noy, ambaye ni msemaji wa hospital ambayo alikuwa amalazwa Sharon alisema " matibabu ya kila aina yalifanyika ili kummponya Sharon, lakini haikuwezekana na hivyo hatupo naye tena."

Msemaji wa familia ya Areal Sharon, Yoram Ravid amesema " kwa kuwa Sharon alikuwa ni mwanajeshi na hivyo naimani mazishi yake yafafanywa kwa taratibu za kijeshi."

Areal Sharon, atakumbukwa kwa hisia tofauti, kwa wengine kumwita shujaaa na wengine muuaji.

Kufuatia kifo cha Areal Sharon, Viongozi mbali mbali duniani wametuma salamu zao za rambi rambi kwa watu na serikali ya Izrael.

No comments: