Msemaji mmoja wa kundi hilo, bwana Pasteur Habimana, amedai wamewateka nyara mafisa wawili, mmoja ni afisa usalama wa jimbo la Cibitoke, na afisa wa polisi anaye shughulikia uchunguzi na usalama wa Bujumbura.
Msemaji huyu aliongeza kwa kusema, wameaua kufanya hivi, ili serikali iwapatie wanachama wao ambao wamafungwa katika majela ya serikali.
Pichani hapo juu ni askari wa jeshi la serikali wakiwa kazini , na chini ni picha ya askari wa serikali akiangalia miili ya watu walio kufa, baada ya mapambano na wapinzani wa serikali wajulikanao kama The Force of National Libaration (FNL)
Serikali yarudi nyuma, walala hoi"Chingas warudi mitaani"
Dakar. Senegal -Baada ya serikali ya Senegal kujaribu kuwafukuza,wafanya biashara wadogo wadogo wanao uza mitaani, hasa ndani ya jiji la Dakar kwa kutumia nguvu zake za dola, imeamua kuruhusu tena wafanya biashara hawa kuendelea na biashara zao kama kawaida.
Kufuatia maelezo ya benki ya dunia,asilimia 95% ni wafanyakazi wadogo wadogo(Chingas),na kunapunguza uzururaji na ukosefu wa kazi nchini humo.
Pichani ni mwela wa kupambana na vurugu, wakiwa wanamalizia kazi yao ya kuwafukuza (Chingas), kabla ya kruhusiwa kurudi mitaanai kuendelea na biashara zao kama kawaida.
Polisi wa Brazil, wachanganya madawa,"Msicha wa miaka 15 aona cha moto."
Sao Paulo. Brazil -Kutokana na wingi wa uarifu, unaosababishwa na ukosefu wa kazi, kumepelekea kujaa wa watu walio fungwa jela.
Hali hii imesababisha, polisi kwenye jimbo moja la Para, wamefanya kitendo cha kushutua jamii ya wa Brazil na ulimwengu kwa ujumla, baada ya kumuweka mahabusu msichana mmoja wa miaka 15 na wafungwa wengine wa kiume wapatao 20.
Kutokana na kitendo hicho, cha polisi kumweka pamoja na wanaume kulipelekea msichana huu kubakwa na kunajisiwa na mahabusu wenzake wa kiume.
Uchunguzi wa kesi hii bado unandelea, na wote walio husika na uzembe huu watachukuliwa haua, msemaji wa polisi alisema.
Hapo juu ni picha za lupango nchini Brazil,ambazo zinasadikiwa kujaa, huduma ni duni.
Mimi na wewe mpaka milele, lakini siyo kama ilivyo. " Nchini Misri"
Cairo.Egypt - Zaidi ya ndoa 240, huwa zinavunjika,au wapendanao kuachana, hii ni kutokana na na achunguzi wa maswala ya jamii.
Hii ni kuwa kila siku, ndoa moja huvunjika kwa kipindi cha dakika sita (6), kwa kipindi cha mwaka wa kwanza wa ndoa, na kukadiriwa ya kuwa kuna idadi ya ndoa 2,5 millioni kwa mwaka huvunjika.
Wengi ya wanaodai taraka ni wanawake,au kupewa taraka na waume zao kutokana na sababu mbali mbali, hasa wanaume wengine kutaka kuongeza mke mwingine ndani ya nyumba.
Ingawaje kuvunjika kwa ndoa huchukua muda, hasa kuzingatia muda wa kufatilia uamuzi wa mahakama.
Lakini msemaji alisema ya kuwa kunandoa nyingi, ambazo huvunjika bila habari zake kujulikana.
Hapo juu ni vifungo ya chuma vya maisha ambavyo wapendanao huwa wanafungana ili waishi milele, lakini mara wanakata kwa msumeno vifungo hivi...................................... mambo yaha
Australia yapata waziri mkuu mpya, je vita Iraq mashakani?
Sydney. Australia -Waziri mkuu wa Australia bwana John Howard,ameshindwa kupita kuwa tena waziri mkuu wa nchi hiyo kwa kipindi kingine.
Bwana Howard ambaye ameiongoza Australia kwa kipindi cha miaaka 11 kama waziri mkuu chini ya chama chake Liberal Part .
Matokeo ya uchaguzi huu, yamepa bwana Kevin Rudd ushindi mkubwa na kuchaguliwa kuwa waziri mkuu mpya wa Australia baada ya chama chake cha Labor Part kushinda kura, kwa asilimia 53%, zidi ya chama cha cha bwana Howard ambacho kimepata asilimia zipatazo 47%.
Bwana Kevin amehaidi kuleta mabadiliko, na kuangalia upya kuhusu vita vya Iraq.
Pichani ni picha mbili tofauti, picha ya juu anaonekana bwana Kevin Rudd, akiangalia kwa tabasamu baada ya mataokeo.Picha nyingine anaonekana bwana John Howard aki waaga wanachama wenzake baada ya kukubali mtokeo ya uchaguzi
Nimeishi kwa kunywa aja ndogo na majani ya pori"Mfanyakazi wa mbuga za wanyama"

Nairobi.Kenya - Mfanyakazi mmoja, anayefanayakazi kwenye mbuga za wanayama karibu na mlima Kenya uliopo km110 kaskazini mwa mji wa Nairobi, bwana Solomon Nyanjui ameponea chupuchupu baada ya kuanguka na helikopta.
Bwana Solomon Kinyanjui, ambaye ni mfanya kazi wa Kenya Wildlife Service (KWS), amekuwa ana fanya kazi ya kuendesha helikopta, kwa kipindi cha miaka 27.
Baada ya ajali kumkuta, bwana Solomoni Kinyanjui, alisema, aliweza kuishi porini na majeraha, na kwa kula majani na mkojo wake mwenyewe hadi hapo wanajeshi wa jeshi la Kenya walipo kuja kumuokoa.
Hii ni mara ya pili bwana Kinyanjui anaponea chupuchupu,mara ya kwanza alipata na ajali kama hii 1995 wakati alipo kuwa akikagua mbuga za wanyama.
Pichani, ni mmoja wa kifaru, ambaye bwana Solomon Kinyanjui na wafanayakazi wenzake huwa wanawalinda, na kuwafatilia kwa makini ili wasimalizwe kabisaa, na wawindaji haramu ambao huwaua na kuchua pembe zao tayari kwa mauzo.
Zim dolla, kuchapishwa upya, Irani na Zimbabwe ushirikiano wa mzuri zaidi.
Harare. Zimbabwe - Gavana wa benki kuu ya Zimbabwe, bwana Gideon Gono, ametangaza ya kuwa serikali, imetoa noti mpya, hivi karibuni.
Hali hii inakuja, kutokana na kushuka kwa thamani ya pesa ya Zimbabwe, ijulikanayo kama Zimbabwe dollar.
Akiongea na waandishi wa habari, gavana Gideon Gono, lindelea kwa kusema kwa kuwashutumu baadhi ya wafanya biashara na wale watu wanao shikilia pesa, wanaombwa wa zibadilishe kwa haraka, kabla ya kupoteza thamani yake, na akaagiza benki ziongeze maasaa, ili kukabiliana na mabadiliko haya.
Wakati huo huo, ushirikioano wa Zimbabwe na Iran unazidi shamiri,baadaya viongozi wa nchi hizi mbili kukutana na kuongea wakati rais Robert Mugabe, alipo tembelea hvi karibuni nchin Iran.
Pichani ni rais wa Iran, Mahamoud Amadinejad na rais Robert Mugabe, wakikagua gwaride rasmi lillilo andaliwa kwaajili ya rais Mugabe.
No comments:
Post a Comment