Saturday, November 17, 2007

Pakistani yaibuka mshindi." Ya ngoswe wa mwachia ngoswe .

Mfalme wa tenis bado kuwa yule yule, hakuna wa kumshinda kwa sasa.

Shangai. Mchezaji wa tenis bora duniani Roger Federer amezidi kuonyesha umaili wake baada ya kushinda mpinzani wake mkuu kutoka Spaini David Ferrer kwa pointi 6-2,6-3,6-2. Mechi hiyo iliyo chukua dakika zipatazo 98. Dakika hizi zilikuwa kama moto kwa bwana Ferrer, na kumpa nafasi Feder kushinda kikombe hiki kwa mara ya pili. . Pichani hapo juu anaonekana Roger akishangilia kwa nguvu baada ya kushinda mechi mjini Shanghai. Na picha nyingine Roger na Ferrer wanaingia uwanjani huku muziki wa nguvu ukiwasindikiza kumenyana kwenye kinyanganyiro hicho ambacho Feder alibuka na ushindi na kudhihilisha ni mwamba wa tenis. Pakistani yaibuka mshindi , Ya ngoswe wa mwachia ngoswe.
Islamabad. Timu ya kriketi ya Pakistani imezidi kuimarisha ushindi wake , baada ya kuwashinda waasimu wao wakuu India na kuonyesha ya kuwa michezo na siasa ni njia mbili tofauti.
Nyota mpya ya Pakistani katika mchezo huu wa kriketi, bwana Shoab Malik, ndiye aliye kuwa mwiba kwa wana kriketi wa India baada ya kushinda ponti nyingi ambazo ziliwawezesha Pakistani kushinda kwa mizunguko 3 na India mizunguko 2.
Hapo juuu anaonekana nyota ya timu ya kriketi ya Pakistani bwana Shoab Malik akipongezwa na wenzake baada ya kushinda pointi nyingi zaidai ya wachezaji wote katika mpambano huo..
Hali ya hatari itakuwepo mpaka hali itakapo kuwa shwari" Rais Gen Musharraf"
Naibu katibu mkuu wa Amerika , bwana Negroponte, amemwomba, rais Gen Musharraf , kuondoa hali ya hatari ailiyo iweka nchi nzima.
Negroponte aliyasema hayo alipo kutana na rais Gen Musharraf, hivi karibuni wakati naibu katibu huyu alipo tembelea kikazi nchini Pakistani ili kutatua mgogoro wa kisiasa uliopo kati ya rais Gen Musharraf na wapinzai wake wanao ongozwa na bibi, Bhuto.
Hata hivyo rais Gen Musharraf ali haidi ya kuwa tarehe 9 january ni siku ya uchaguzi nchini Pakistani, na kuhaidi kuendelea kupigana na magaidi wote waliopo Pakistani.
Rais Gen Musharraf,amesema kuweka amri ya hali hatari , nikataika kurudisha utulivu na amani nchini humo, na halia hii iata tolewa pindipo hali itakapo kuwa shwari.
Pichani hapo juu ni bwana Negroponte,alipo kuwa akiongea na waandishi wa habari.

Ugonjwa wa ajabu wauwa na kuacha kitendawili nchini Angola.

Luanda. Shirika la afya ulimwenguni,WHO limetangaza ya kuwa, ugonjwa usiojulikana ambao uliibuka nchini Angola, huenda umesababishwa na sumu.
WHO, imesema bado inafanya uchunguzi zaidi ili kupata utatuzi wa madhara haya, kwani mpaka sasa watu wapatao 368, wamesha ugua kutokana na sumu hii, na wengine wa 6 wamasha aga dunia
Bado yupo imara, yote yamekuwa muruha- (gado),"Msemaji wa Wackojaco"
Califonia. Mwana muziki maarufu wa muziki wa pop na kuruka majoka Michael Jackson, amaepuka kupoteza eneo na nyumba yake Neverland.
Hali hii ya kupoteza Neverland ilikuja baada ya habari kuvuma ya kuwa kwa sasa Michael ana pambana na ukwasi.
Lakini msemaji wa Michael,amesema ingawaje eneo hili Neverland lili kuwa katika utata, lakini utata huo umekwisha
Michael Jackson, ambaye tangu kuisha kwa kesi amekuwa akiishi Ireland,Dubai na Las Vegas. Pichani hapo juu ni Michael kwa sasa ,na picha nyingine chini ni Michael enzi hizo mwaka 47
Wakadogo wakombolewa na Unincef,hali yadizi kuwa mbaya. "UN"
Kinshasa.Chirika la kuhudumia watoto Unicef, limesema limekomboa askari watoto wapatao 232 kutoka kwenye makundi yanayo pigana nchini Kongo.
Watoto hawa ambao walikuwa maaskari, wengi wametoke kundi la Mayi mayi lililopo kusini mwa mji wa Kivu
Kukombolewa kwa watoto hawa, kumekuja kutokana na msaada wa UN na vyama vingine vya kusaidia watoto.
Kutokana na msemaji wa Unicef, amesema kutokana na vita vilivyo ibuka hivi karibuni, ongezeko la watoto kufanywa askari kunazidi kuongezeka
Pichani hapo juu ni askari watoto wakiwa wameshika mitutu,kushiriki kwenye vita vinavyo endelea mpaka hivi sasa.
Uzembe na kuto wajibika kwa waganga wa hospitali. "Wachangaya madawa".
Dare es Salaam.Waziri wa afya wa erikali ya Tanzania ameomba msamaha kwa familia na wananchi kwa ujumla baadaya ya upasuaji wa kimakosa ulio fanyaika katika hospitali kuu ya Muhimbili.
Uzembe huu ulifanywa na waganga wa upasuaji hospitalini Muhimbili iliyopo jijini Da er Saam, kwa kumfanyia upasuaji wa kichwa bwana Emanuel Didas, badala ya upasuaji wa goti.
Pichani ni bwana Emmanuel Didas akiwa amepumzika kitandani baada ya upasuaji wa kichwa.
Wala mirungula na kudai kitu kidogo kaeni chonjo" Sierra Leone"
Freetown. Rais mpya wa Sierra Leone, bwana Ernest Bai Koroma amepishwa hivi karibuni na kuhaidi kupigana na rushwa kwa kutumia kila aina ya siraha.
Bwana Ernest Bai Koroma, alisema inatakiwa kwa kipindi cha miaka mitatu ya kipindi cha utawala wake lazima kuwe na mabadilko na maendeleo, na hali za watu lazima zibadilike.
Aliwaagiza polisi waache mchezo wa kuomba kitu kidogo kwa raia, na walimu wasiwanyase wanafunzi kwa kuwalazisha kuwafanyia biashara. Hapo juu pichani ni bwana Ernest Bai Koroma wakati wa kampeni zake za kuwania kiti cha uraisi.
Joto la jiwe la Kisomalia kuwageukia wanajeshi wa AU" Sheikh Aden"
Mogadishu. Kiongozi wa wapinzani wanao pinga serikali ya mpito nchini Somalia Sheik Aden Hashi Ayrow, amewaagiza wapiganaji wake waanze kuwashambulia wanajeshi wa jeshi la Umoja wa Afrika waliopo nchini humo.
Navile vile ame waomba wapiganaji wengine kujiunga na kundi lake lijulikanalo kama Al Shabab
Hali hii imekuwa ngumu kwa serikali ya mpito ya Somali inayao ongozwa na rais Abdullah Yusuf , kujenga nchi ya Somalia ambayo imekuwa na vita vya wenyewe kwa wenye kwa zaidi ya miongo mmoja. Pichani hapo juu wanaonekana maskari na kifaru cha wanajeshi AU wakila doria mjini Mogadishu.
Nyeti za jela ya Guantanamo Bay zimepenyezwa hadharani
New York. Mafaili ambayo yamekusanya siri na jinsi ya kuwatunza wafungwa, ambao wanao ishi au kuletwa kwe jela ya Guantanamo.
Mafaili haya yenye kurasa zaidi ya 238, zimechapishwa kwenye mtandao na zinaonyesha jinsi gani ya kuwatunza wafungwa wanao daiwa ni magadi.
Moja ya nyeti hizi, nikuhusu ni mfungwa yupi anaruhusiwa kutembelewa na wafanayakazi wa msalaba mwekundu na nani hasiruhusiwe.
Kambi ya Guanatanamo ambao ilifunguliwa mwaka 2002,kwa ajili ya kuwaweka kizuizini magaidi wa nao saidia na Al Qaeda au Taliban . Pichani ni wanajeshi wanaolinda jela ya Guantanamo wakila doria ndani ya jela ya G'mo Bay.
Siraha ya kupunguza nguvu ya ondosha maisha ya abiria kwenye uwanja wa ndege Vancovour"Polisi mashakani"
Kanada. Polisi wa uwanja wa ndege wa Vancuvour, wamejikuta katika hali isiyo ya kawaida,baada ya kuu bila kukusudia wakati walipo tumia bunduku inayo tumia mionzi ya umemem kumtuliza raia mmoja wa Polandi bwana, Robert Dziekanski aliyekuwa na miaka 40.
Bwana, Robert Dziekanski ambaye alikuwa ana elekea nchini Kanada kuuungana na mama yake anayeishi na kufanya kazi jimbo moja lilipo magharibi ya mji wa British Columbia.
Hapo juu wanaonekana polisi wakiwa katika haakai za kumuliza marehemu Robert Dziekanski.
OJ Simpson, kizimbani tena kwa kutuhumiwa kutumia nguvu na siraha.
Nevada, Las Vegas, mchezaji wa zamani wa Amerikani football, OJ Simpson, na wenzake wanne wanakabiliwa na mashitaka ya kuchukua vitu kwa nguvu,kutoka kwenye duka mmoja karibu na kasino mjini hapo, amabalo linauza vitu vya wachezaji wa zamani na maharufu wa Kiamerika.
OJ Simpson, alikwenda kwenye duka hilo, kuchukua vitu vyake alivyodai ya kuwa viliibiwa kutoka kwenye makazi ya bwana OJ Simpson, na mwenye duka hilo ndiye aliye vinunua, na vilikuwa kwenye duka hilo.
Lakini mwenye duka hilo alidai OJ na wenzake walitumia nguvu na walikuwa na mitutu, an waitumia mitutu hiyo kuwatishia.
Hapo juu ni bwana OJ Simspson akiwa anaangalia kwa makini jinsi mwanasheria wake anavyo ongea.

No comments: