Wednesday, November 21, 2007

Tumeshikwa na mshangao, butwaa na mshituko" Wafanyakazi wa CNN"

Baada ya kuonja lupango tena, natubu makosa yangu" Mike Tyson"

Bingwa wa zamani wa ndondi wa dunia, Mike Tyson, amemaliza kifungo cha siku moja jela.
Tyson, alihukumiwa kifungo hiki baada ya kukamatwa na mihadharati na kuendesha gari, wakati akiwa amelewa na alikubali makosa haya kabla ya hukumu hiyo haijatolewa.
Hata hivyo Mike Tyson mwenye miaka 41, kumalizia kifungo hicho, siyo mwisho wa hukumu, bali itambidi atumike bwelele(bure),kwenye maeneo ya umma kwa masaa 360 kadha, ili kumalizia adhabu hii.
Pichani ni Mike Tyson, alipokuwa amudhulia tafrija moja mjini Mesa, Arizona, kabal ya hukumu hiyo.
Sampras ang'ala, lakini nyota ya sasa yazidi kung'ara"Tenisi"
Seoul. Bingwa wa zamani wa dunia wamchezo wa tenisi, Peter Sampras, alishindwa kuonyesha umail wake.
Sampras, alishindwa vibaya,na bingwa wa sasa wa dunia wa mchezo wa tenisi Roger Federer, ambaye alitawala vipindi vyote viwili vya mchezo huu kwa kushinda 6-4 6-3 machezo uliyo chukua dakika zipatazo 60.
Wakiongea na waandishi wa habari baada ya mcheo huu, Sampras, alisema kwa pande wake ni kwamba anafurahi kwani alicheza vizuri kwa kiwango chake, ingawaje uzito wa mwili bado una mletea utata kiasi, na kuahaidi mechi ijayo, ambayo watarudiana anaweza fanya mavitu yake.
Na kwa upande wa Feder, alisema amefurahi kwa kucheza na bingwa wa zamani, na Sampras ame dhihilisha ya kuwa alikuwa nyota enzi zake alimalizia kwa kuseama Federer.
Pichani hapo juu, anaonekana akifanya vitu vyake alipo pamabana na Federer.
Wanasiasa wa Ulaya Magharibi wanataka kuichafua nchi yetu" Rais Putin"
Moscow. Rais wa Russia, Vladamil Putin, amewashambilia, wanasiasa wa ulayamagharibi, kwa kuingilia maswala ya kisiasa ya nchi ya Russia, wakati wa kampeni za uchaguzi wa wabunge ambao utafanyika dec, 2-2007.
Rais, Putin alisema ya kuwa wanasiasa wa ulaya magharibi wanataka kudhoofesha hali ya nchi.
Kampeni hii, ambao rais Putin,ana ongoza chama chake cha United Russia, kinatarajiwa kushinda.
Walio kuwa na makosa,na watendaji wakati wa ubaguzi wa rangi wasamehewe"Rais Mbeki"
Cape Town. Rais wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki, amesema ya kuwa watu ambao waliofanya makosa ya kisiasa kabla ya 1999, wakati serikali ya ubaguzi wa rangi, anaweza kuomba kupata msamaha.
Rais Mbeki, alisema kufuatia na hali hii, ambayo haikuisha, wa katia wa kusema ukweli na kusamaeheana( Truth and Renconciliation),ambayo iliwekwa ili kusameheana, ili kujenga upya Afrika ya kusini.
Kamisheni, liyokuwa ikiongozwa na wa kanisa la Kingrikana nchini Afrika ya Kusini, askofu Desmond Tutu iliwasamehe watu wapatao 1000 ambao walifanya makosa wakati ya serikali ya Ubagizi wa rangi. Rais Mbeki, alisema watu hawa, wanatakiwa uanza kuomba msamaha kuanzia januari 15, 2008, na kabla ya msamaha uhuu kutolewa, mazungumzo yatafanyika kwa wahusika wote.
Hapo juu, ni picha ya rais, Thabo Mvuyelwa Mbeki,ambaye anakaribia kumaliza muda wake kama mwenyekiti wa chama tawala ANC ( Afrikcan National Congress).
Tumeshikwa na mshangao, butwaa,na kustuka,"Wafanyakazi wa CNN"
Atlanta.Daktari aliye usika katiak upasuaji wa mama ya mwana muziki, Kanye West, Dr Jan Adam, alikatisha mahojiano na mtangazji maarufu wa CNN.
Mahojiano hao yaliyo takiwa kufanyika katika studio za CNN Atlanta, kati ya Dr Jan Adam na bwana Larry King, yalisimama baada ya Dr Jan Adama kupata ujumbe ya kuwa asimamishe nahijiano hayo, ambayo yange husu hali halisi kuhusu upasuaji wa wa marehemu Dr Donda, mama ya mwana muzuki maarufu Kanye West.
Hali hii ili washangaza na kuwashutua wafanyakazi wa CNN, hasa bwana Larry King, kwani walikuwa wameshajiandaa kwa matangazo haya.
Pichani ni Dr Adam akitoa kiongela sauti( Microphone) tayari kunyanyuka kutoka ndani ya studio ya CNN Atlanta.
Fungueni mipaka ya Afrika Mashariki kwa muda wa masaa 24 kila siku.
Kampala. Rais, Poul Kagame ameziomba nchi wanachama wa jumuia ya Afrika mashariki, kuwa na mpango maalumu wa kufungua mipaka kwa muda wa masaa 24.
Rais Kagame aliendelea kwa kusema, ya kuwa kutokana na hali ya uchukuzi na barabara, inakuwa ni vigumu kwa wafanya biashara, na magari yanayo beba mizigo, kwani usafirishaji huchukua siku tatu hadi tano kabala ya kumfika kule unapo hitajika.
Na ameomba kulegeza mashariti katika sekta tofauti, ili kuweza kuajili watu wenye ujizi kataika kila nchi.
Aliongezea kwa kusema ya kuwa, hivi sasa nchini Rwanda, watu wenye ujuzi na wataalamu, wanapewa kipao mbele na hakuna vikwazo tena.
Na hii inasaidia kukuza soko la kazi na biashara pian aliyaongea haya alipo kuwa akihudhuria mkutano wa kibiashara ulioandaliwa na rais wa Uganda bwana Joweri Kaguta Mseven.
Kuba bado ni mshiriki muhimu wa Afrika, katika nyanja zote za kimandeleo.
Gaberone.Serikali ya Botswana na serikali ya Kuba zimesaini mkataba wa , kibiashara, uchumu, sayansi, elimu, ufundi,michezo na afya
Akiongea wakati wa kuadhimisha miaaka 30 ya ushirikiano, balozi wa Kuba , bwana Jorge Tormo, alisema uhusiano huu wa nchi hizi mbili, umeleta maendeleo kwa pande zote, hasa kataka sekta ya elimu na afya.
Baada ya miongo minne kupita, Malkia akanyagatena ardhi ya Uganda.
Kampala.Mkutanao wa nchi wanachama wa (Commonwealth) au nchi zote zilizokuwa koloni la Mwingereza, ziananza mkutano wa pamoja kuzungumzia, maswala ya kijamii , kisiasa ,na kiuchumi.
Uganda ambaye ndiye mwandaaji wa mkutano huu ambao utafunguliwa na Malkia wa Uingereza, malkia Elizabeth II siku ya ijumaa.
Malkia ameshawasili nchini Uganda tayari kwa ufunguzi huu.
Malkia Elizabeth II, kwa mara ya mwisho alikuwa nchi 1954, kabla ya Uganda aijapata uhuru.
Malkia ameongozana na mumewe Prince Philips the Duke of Edinburg.Prince Philips ambaye 1954 aliongozana na Malkia Elizabeth, walipoembela Uganda wakati uo.
Pichani juu anaonekana rais Yoweli Kaguta Mseven, akiangalia maandalizi ya mkutano kama yana enda sawa.

No comments: