Wednesday, November 28, 2007

Mazungumzo, au kuongea,ni dawa ya kumaliza uhasama"Korea,Kusini/Kaskazini.

Nyota ya Denzil Washigton yazidi kung'ara, "kumbi za sinema kurindima".

New -York. Amerika . Mcheza sinema, bora na maarufu duniani Denzil Washington, ametokea kuwa kipenzi cha watazamaji wa sinema ulimwenguni. Denzil Washington, ambaye amcheza sinema inayoitwa American Gangstar, ambayo hadi hivi sasa, ndiyo gumzo la wapenda sinema. Akiongea katika ufunguzi wa maandalizi ya sinema mpya itakayo julikana Great Debaters, mmoja ya wasimamizi wa sinema hii, amesema nyota ya Denzil Washington itazidi ngara. Sinema hii Great Debeters inatarajiwa kuingia kwenye kumbi za sinema muda si mrefu. Kwenye sinema hii, itaelezea hali halisi na jinsi gani 1930s mambo yalivyo kuwa enzi hizo. Denzil Washington amshinda zawadi nyingi za kimataifa kama mcheza sinema, Denzil Washington alizaliwa ndani ya Jijini la New York. 28/12/1954. Kocha mkuu na mkurugenzi wahojiwa na polisi" Mirungura na kabumbu". London, Uingereza - Kocha mkuu wa Portsmouth, bwana Harry Redknap na mkurugenzi wake mkuu, wamekamatwa na polisi , kwa ajili ya mahojiano. Viongozi hawa wa Portsmouth, wanashukiwa kuhusika katika ulaji mrungura,wakiwemo watu wengine hambao mpka sasa majina yao hayajulikani. Msemaji mmoja wa polisi,alisema msako huu, ni moja katika uchunguzi unaoendelea kuchunguza mirungura katika kabumbu. Hapo juu ni kocha mkuu wa Portsmouthm Harry Redknap, akiangalia kwa makini wakati timu yake ikipambana moja ya lgi zinazo endelea nchini Uingereza.
Hali bado ngumu vita zidi ya Taleban, ajari katika mapambano.
Kopenhagen,Denmark- Ofisi ya jeshi la ulinzi, nchini Denmark, imesema ya kuwa wanajeshi Uingereza, wamewaua wanajeshi wa jeshi la Denmark.
Vifo vya wanajeshi hawa vilitokea september 26, wakati walipo shambuliwa na na wanajeshi wa uingereza, katika harakati za kupambana na askari wa jeshi la Taleban
Msemaji mmoja wa jeshi, alisema bado uchunguzi unaendelea kuhusu tukio hilo.
Nawakai huo huo, wanajeshi wa jeshi la Amerika, wameshambulia basi dogo lililo kuwa limebeba wafanyakazi wa benki, ambao walikuwa wakielekea kazini.
Msemaji wa jeshi la Amerika, alisema tukio hili, lilitokea maeneo ya Shaab kaskazini ma Baghdad.
Tukio hili, limekuja wakati serikli ya Iraki, ina jadili jinsi gani kushirikiana na jeshi la Amerika ili kupunguza matukio kama haya yasiongezeke.
Pichani, ni askari( wanajeshi) wa NOTO, wakiwa mstari wa mbele kupambana na Taleban.
Mazungumzo au kuongea, ni dawa ya kumaliza uhasama"Korea. Kusini/Kaskazini.
Seoul,Korea Kusini - Serikali ya Korea ya Kusini na Serikali ya Korea ya Kaskazini, zimeanza mazungumzo, katika kuboresha uhusiano, mbao zaida ya miongo mitano zimekuwa zi uhasama.
Mazungumzo hayo yatawakutanisha, waziri wa ulinzi wa Korea ya Kusini bwana Kim Jang-soo ,
mkuuwa maswala ya usalama wa Korea ya kaskazini bwana Lee Jee-joung.
Katika ziara yake bwana Kim Jang-soo na Lee Jee-joung,wataongelea jinsi ya kutatua mgogoro wa mpaka unaotenganisha nchi hizo mbili, na atatembelea maeneo ya viwanda.
Uhasama huu,wanchi hizi mbili ulianza baada ya kusaini mkataba wa amani mwaka 1950-53, baada ya vita kuisha katika njia isiyo yakawaida.
Pichani anaonekana waziri wa ulinzi wa korea ya Kusini bwana Kim Jang - soo alipokuwa anaelekea Korea ya Kaskazini, huku akiashiria kwa dole gumba ya kuwa mabo yote yatakuwa mazuri.
Ukweli umweka mtu huru,ujanani nilifanya mambo haya"Baraka Obama".
Washingtone. USA - Mgombe wa kiti cha urahisi, kupitia chama cha Demokratiki, nchini Amerika, bwana baraka Obama, amekubali ya kuwa alishawahi kutumia madaya ya kulevya wakati wa ujana wake.
Akizungumza wakati wa kampeni ya uchaguzi, bwana Obama alikubali ya kuwa wakati yupo sekondari alisha wahi kutumia madawa ya kulevya, na anajuta ni kwanini alifanya kitendo hiki.
Bwana, Baraka Obama, aliongeza kusema ya kuwa umri wa ujana, wakati mgumu saaana, kwani unaweza fanya mambo ambayo huja ukajuta baadaye.Lakini ni vizuri kueleza ukweli, kwani hta rasi Billy Clinton, alikubali yakuwa ujanani aliwahi kutumia au kuvuta mjani(marijuana).
La muhimu ni kuacha tabia hiyo kabla ujahathirika na maisha ya baadaye.
Pichani ni picha ya bwana Baraka Obama, alipo kuwa akijibu maswali wakati wa kampei ya uchaguzi, mjini Hampshire.
Uingereza na Robert Mugabe,moto wazidi kukolea.Nani wa kuuzima?
London, Uingereza - Waziri mkuu wa Uingereza bwana Gordon Brown, amesema hatahudhuria mkutano ,utakao kutanisha viongoozi wa Afrika na Ulaya, mwezi wa desemba.
Bwana Brown,alisema haya baada ya rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, kuhaidi ya kuwa atahudhulia mkuto huu.
Nia na madhumuni ya mkutano huu, kudumisha uhusiano kati ya bara la Afrika na Ulaya. Lakini hata hivyo, rais wa Umoja wa Ulaya, bwana Jose Barroso, alilisitiza mazungumzo ndiyo suruhisho la kila jambo ,na siyo matatizo ya kibinafsi.
Vile vile wajumbe wa Umoja wa Ulaya, wanona ya kuwa mkutano huu, utazidi kukuza uhusianao uliopo ka ya Afrika na Ulaya kiuchumi na Kijamii. Hapo juu pichani ni waziri mkuu wa Uingereza, bwana Gordon Brown, aliye susia kuhudhulia mkutano utakao fanyika nchini Ureno.
Hakuna "Sharia laws" Uchaguzi wa ibuka na maswala ya dini.
Nairobi, Kenya - Shirikisho la Waislamu nchini Kenya, limekanusha vikali ya kuwa, chama cha upinzani nchini Kenya, kinacho ongozwa na Raila Odinga, pindipo kikishinda uchaguzi unaotarajiwa kufanyaika mwezi wa desemba 2007, kita ruhusu maeneo fulani ya nchi Kenya kuwa na Sharia Law."Amri za kisharia".
Msemaji mmoja wa shrikosho hilo amesema hayo, baada ya viongozi wa dini ya kikristu, kutaka kujua kama habari hizi ni kweli.
Hii inakuja baada kuhaidi kulinda na kufuatili upya jinsi gani watu ambao ni wafuasi wa dini ya Kislamu wanavyo nyimwa baadhi ya haki zao, na vilevile matokeo ya kura za maoni kuonyesha ya kuwa bwana Odinga yupo, mbele kwa 45% zidi ya mpinzani wake rais wa sasa bwana Mwai Kibaki.
Nchni Kenya watu amabo ni wafuasi wa dini ya Kislamu wengi wao wanaishi maeneo ya Pwani ya Mombasa, Lamu na wachache wapo kanda za nyanda za juu.
Pichani ni waumini wa dini ya kislamu nchini Kenya wakiwa wana omba Mungu msikitii.
Wazee wa Afrika waliotimiza malengo yao,mengine yalikuwa ya ziada, kwa ubaya na kwa uzuri.
Hapo juu, ni wazee wetu wa kwanza kujua kutea haki na tamani ya mtu,katika ulimwengu wa sasa, walipigania uhuru, kwa kila namna, nakuhakikisha ya kuwa Afrika imekuwa huru.
Ijapokuwa walipo kuwa wakipigania uhuru, walikuwa na nia tofauti,jambo la maana walilo fanya ni kuakikisha kila mtu, atokeae Afrika, anakuwa huru, uweza wa kisiasa,au wakiuchumi.
Hawa viongozi wa kwanza wa Afrika, walipambana na mambo mengi,hasa kwa kuzingatia mazingira yaliyo kuwepo wakati ule.
Kitu ambacho wana wa Afrika, "hasa viongozi wa sasa", tunapashwa kujua yakuwa deni tulilo nalo ni kubwa saana, kwani viongozi hawa waliweka na kujitolea maisha yao ili kila mwafrika awe huru na kuleta usawa kwa wote.
Kama inavyo eleweka, kila binadamu anaasili ya uchoyo na uoga,awe kiongozi au raia wakawida, awe mwafrika, mzungu, mchina, au watu kutoka bara la Asia na Amerika.
Hii inategemea ni kwa kiasi gani uchoyo na uoga huu anaweza ukaishinda nafsi ya mtu.
Hali huwa ni mbaya hasa, inapotokea, mtu,watu,au kundi la watu, (aliye)au walipoewa uwezo na Baba Mola, kuwaongoza watu wenzao, kushindwa kujizuia hii tabia ya uchoyo na woga, na hapo huwa ndiyo chanzo chakuwa na matabaka,ya walio nacho na wanaotafuta kila siku.
Jambo la muhimu lazima tukumbuke, viongozi hawa wa Afrika waliotetea na kupigania uhuru, lengo lao kuu, walilikamilisha, na ndiyo maana, leo hii kila Mwafrika anatembea kifua mbele, macho mita mia.
Ni kweli, viongozi hawa walipo kamirisha kazi zao za kupigania uhuru,iliwabidi waanze kupambana na hali halisi ya kuichumi na ongezeko la watu katika kila nchi ya Afrika.
Hali hii ilipelekea jamii, kuanza kuulizana ni kwanini,mambo yanaanza kubadilika.
Tukiangalia kiundani, siyo kama viongozi hawa, hawakujua haya matatizo haya, lakini hawakuwa na mbinu mpya za kutatua matatizo haya.
Kipindi cha kupigania huru wa Afrika , dunia nzima kwa ujumla ilikuwa na wakati wa mageuzi, tukiangalia Ulaya ilikuwa inajijenga taratibu baada ya vita vya pili vya dunia, Amerika ilikuwa ian zidi kujiimarisha kwa kuwekeza vitega uchumi karibu dunani kote., kujenga uhusianao mzuri na bara la Ulaya.
Kwa kweli kipindi cha miaka ya 60s, kilikuwa kipindi cha nani anaupeo zaidi wa kuonambele, ili kumtumia mwingine kwa manufaa yake.
Wakati viongozi wa Afrika, wanafikiri nini la kufanya, dunia na walimwengu wakawa wanabadilika kimawazo, kivitendo kila kukicha, na kukatoke vishawishi ya kila namna irimradi (kila mtu),au nchi ipate inacho ona kitanufaisha jamii yake na wananchi wake.
Vile vile lazima tukumbuke, ya kuwa binadamu yoyote, awe, mwafrika, mzungu, mwarabu, mchina, muhindi au kutoka jamii yoyote, akitaka au kunia kitu, atatumia kila mbinu, vitisho, ulaghai,na kuua ili afaikiwe malengo yake.Ya huyu ndiye binadamu alivyo.
Kutokana na hayo yote, ikapeleka, baadhi ya viongozi wa Afrika, kushindwa kujizuia na tabia ya uchoyo na uoga, naikawa raisi kusahahu na kukumbuka nini walihaidi wakati wa uhuru.
Kwa kuona hivyo, (watu)au nchi ambazo zilikuwa zina hitaji kujijenga, zikapata mwanya wa kuendelea kujijenga zaidi, kwa kutumia mbinu zote walizoona zinafaa kupata mandeleo na hali hii inaendelea mpaka leo hii katika kila jamii.
Hii yote isiwe sababu, inabidi tuelewe ya kuwa, hasili ya binadamu anaependa kwanza apate yeye, na ndiyo ataweza kuangalia mwingine kama anacho cha kutosha.
Na hii inamaanisha ya kuwa hatuna haja ya kulaumiana, kwa kushutumumiana, kwani wanabinadamu wamebarikiwa na Baba Mola, kuwa na mtu au watu fulani ambao wataweza kuwaongoza wenzao, ili waweze kuwajenga kimaisha, kiuchumi na kifikra hapa duniani.
Swali la kujiuliza Je viongozi wa sasa, wanaweza kujitolea kupoteza maisha yao? Kama walivyofanya viongozi waliopigania uhuru. Je viongozi hawa wasasa wanatimiza majukumu yao ya kupenda na kujenga vya kwao, na nchi zao?
Lazima kujifunze ni jinsi gani tutatue makosa yaliofanywa na viongozi wetu siyo kubakia kuwa na choyo na woga, ambavyo ndiyo chanzo cha matatizo yote yaliopo.
Viongozi hawa waliopigaia uhuru walitimiza lengo lao, mengine yaliyo tokea baadaya ya uhuru yalikuwa ni ya ziada, mazuri kwa mbaya.
Viongozi wote dunia, kumbukeni, yakuwa mnalakujibu mbele ya Baba Mola, kama hamkutimiza yale yote yaliyo pashwa myatimize kama viongozi, kwani mpaka leo, hakuna aliye rudi kutuelezea huko wanapokwenda watu milele, kuna nini.
Ni bora tuamini Mungu yupo, kwani tukiaga dunia, natukaenda huku wanapo kwenda watu wengine wasio rudi na tusimkute, ni salama kwetu. Lakini je tukienda tukamkuta yupo tutafanya nini?
Kwani siku zote baba mzuri ni yule anayependa na jenga nyumba yake. Hayo ni maoni ya Muhariri ya kila mwezi. Mungu atubariki.Amina

No comments: