Thursday, April 30, 2009

Jeshi la Uingereza kuanza kurudi nyumbani kuanzia leo.

Rais, Baraka Obama, kafanikiwa alimia 65% kwa muda wa siku 100, ofisini. Washington, Amerika - 30/04/09. Rais wa Amerika, Baraka Obama, ametimiza siku 100,tangu kuwa rais wa Amerika. Kwa mujibu wa wachunguzi wa mabo ya kisiasa na kiuchumi, wanasema rais, Baraka Obama, amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kukamilisha kwa asilimia zaidai ya 65% kwa ya le yote aliyo yasema wakati wakampeni za uchaguzi wa rais mapema mwaka jana. Moja ya mamba ambayo rais , Obama ameyatimiza, ni kufungwa kwa jela, ya Guantanamo Bay,kutia sahii kuzuia kuteswa kwa wafungwa au mtuu yoyote kinyume na sheria za haki za binadamu,kusaidia kuyakwamua kifedha makampuni makubwa ya magari kama GM(General Motors) nchini Amerika na kurudisha uhusiano mzuri na nchi nyingi ikiwemo, Venezuela. Picha hapo juu anaonekna, rais wa Amerika Baraka Obama,akionyasha vidole ya kuwa mambo ni kuelekea mbele, kabla ya kuanza kuongea na waandishi wa habari na kujibu maswali. Jeshi la Uingereza kuanza kurudi nyumbani kuanzia leo. Basra,Irak - 30/04/09.Jeshi la Uingereza limemaliza muda wake wakuu kaa nchini Irak, kama jeshi la ulinzi na kulinda amani. Hii ina fuatia , baada ya ya waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown,kusema haya siku ya alkhamisi wiki hii wakati alipo kutana na waziri mkuu wa Irak,Nour al Maliki, ya kuwa jeshi la Uingereza litajea nyumbani. Jeshi hilo la Uingereza limekuwa nchini Irak kwa kipindi cha miaka sita (6). Kwa mujibu wa habari kutoka kwenye jeshi la Uingereza, zina sema ni wanajeshi 400 watakao baki, kwa ajilii ya kutoa mafunzo kwa Wairak. Picha hapo juu wanaonekana, wanajeshi wa jeshi la Uingereza wakiwa wanatoa heshima zao kwa wanajeshi wenzao waliopoteza maisha katika vita nchini Irak, vilivyo anza mwaka 2003.

Kesi ya mauaji ya waziri kuu wa Lebanoni watuuhumiwa bado kupatikana.
Beiruti,Lebanoni - 30/04/09. Wakuu wa nne wa jeshi la LebanoniMustafa Hamdan,Jamil al Sayyed,Ali al Hajji na Raymond Azar , waliachiwa huru jana, baada ya mahakama ya Umoja wa mataifa inayo shughulikia kesi za vita na mauaji kusema kuwa hakukua na ushahidi wa kutosha ya kuwa wakuu hao wa kijeshi walihusika katika mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Lebanoni, Rafiki Hariri.
Akiongea hayo, Jaji Daniel Franseen, akisoma mbele ya mahamaka mjini Beiruti, kutangazwa kuachiwa huru kwa wakuu hao wa kijeshi,moja kwa moja kwa njia ya runinga (TV), kuliamsha msisimko tofauti kati ya Walebanoni.
Waziri mkuu, Rafiki Hariri, aliuwawa na mabomu tarehe, 22/04/05, na kuleta mvulugano wa kisiasa na kulazimisha kuondoka kwa jeshi la Syria, ambalo lilikuwa nchini humo kwa muda wa miaka 29.
Picha hapo juu, inaonekana picha ya waziri mkuu wa Lebanoni, Rafiki Harii, ikiwa imetundikwa ukutani wakati wa shererhe ya kukumbuka siku ya kifo chake.
Picha ya pili zianaonekana, picha za wakuu wa kijeshi ambao walikuwa wanashitakiwa kwa kuhusika na mauaji ya waziri mkuu, Rafiki Hariri, wameachiwa huru baada ya mahakama kukosa ushaidi kalimi.

No comments: