Wednesday, April 1, 2009

Baraka Obama,ziarani,Ulaya kujadili hali ya uchumi na viongozi wa dunia.

Mkuu wa Taliban, atangaza hali ya hatari kwa Amerika. Washington,Amerika - 01/04/09 - Serikali ya Amerika imetangaz itatoa zawadi ya dola za Kiamerika $ 5 million, kwa mtu atakaye toa habari wapi alipo kiongozi wa Taliban, Baitullah Mehsud, ambaye ametangaza kuwa kundi lake litashambulia Amerika na kuishangaza dunia. Kwa mujibu wa habari zilizo patikana, zinasema yakuwa kiongozi huyo wa Taliban, alisema ya kuwa kundi lake ndili lililo husika na ulipuaji wa kituo cha polisi mjini Rahore, siku ya jumatatu. Baitatullah Mehsud, anashukiwa kuhusika na mauaji ya aliyekuwa waziri mkuu wa Pakistani Bi Benazir Bhutto, na mashambulizi yaliyo tokea katika hotela ya Marriot iliyopo Islamabad. Na inaaminika anauhusiano wa karibu na kundi la Al Qaeda. Picha hapo juu ni ya, Baitullah Mehsud, ambaye anatafutwa akiwa hai au amefariki na serikali ya Amerika kwa kuwekewa zawadi ya US dola $ million 5 kwa mtu atakaye toa habari zake ili akamatwe. Hatimaye Israel yapata waziri mkuu mpya.

Jerusalem, Israel - 01/04/09.Benyamin Netanyahu, ameapishwa rasmi kuwa waziri mkuu wa Israel, baada ya kupata baraka kutoka kwa bunge la nchi hiyo.
Kuchaguliwa kwa Benyamin Netanyahu, kumekuja baada ya muda mrefu wa mvutano wa kisiasa baada ya uchaguzi uliofanyika mapema mwanzo mwa mwaka huu.
Serikali ya waziri mkuu Benyamin Netanyahu, itakuwa na baraza kubwa la mawaziri katika historia ya Israel.
Baada ya kuapishwa kuwa waziri mkuu wa Israel, Benyamin Netanyahu, alisema yakuwa swala la amani na kuundwa kwa taifa la Wapalestina atalipa kipao mbele katika maswala ya kisiasa, uchumi na ulinzi, huvyo kuwataka viongozi wa Palestina wawe tayari kwa ajiri ya kuleta amani kati ya Waisrael na Wapelestina wenyewe.
Picha hapo juu, anaonekana, Benyamini Netanyahu, akiwa anasubiri matokea ya kura ya yeye kuchaguliwa kuwa waziri mkuu wa Israel.
Picha ya pili, wanaonekana,waziri mkuu wa anayetoka madaraka, Ehud Olmert, akimpongeza waziri mkuu mpya wa Israel Benyamin Netanyahu mara baada ya kuchaguliwa kuwa waziri mkuu.
Baraka Obama, ziarani, Ulaya kujadili hali ya uchumi na viongozi wa dunia.
London,Uingereza - 01/04/09.Rais wa Amrika Baraka Obama, ameanza ziara katika nchi za Ulaya na ataudhulia mkutano wa kiuchuni ambao umeandaliwa na waziri mkuu wa Uingereza Gordon Brown.
Wakati walipo kutana na baadaye kuongea na waandishi wa habari, rais wa Amerika Barka Obama, alisema ni muhimu kwa kila nchi kujitahidi kujikwamua kiuchumi, ingawaje itachukua muda na maumivu makubwa katika jamii.
Picha hapo, juu wanaonekana, polisi ambao wapo katika doria ,ili kuhakikisha ulinzi na usalama wa nchi nzima ya Uingereza wakati wa mkutano huu unaotarajiwa kuanza kesho 02/04/09.
Picha ya pili wanaonekna rais wa Amerika, Baraka Obama na mkewe Michel Obama, wakiwasili katika makazi ya waziri mkuu wa Uingereza kabla ya kuanza mazungumzo na kuudhulia mkutano wa kiuchumi.
Latin Amerika na nchi za Kiaarabu, kuongeza ushirikiano wa karibu.
Doha,Katar - 31/03/09.Viongozi Latini Amerika na viongozi wa jumuia nchi wanachama wa nchi za Kiaarabu,wamekutana ili kujadili maendeleo na ushirikiano wakaribu.
Akiongea katika mkutano huo, Mfalme wa Qatar , alisema yakuwa ingawa Latin Amerika na nchi za Kiaarabu zipo mbali ki jiografia lakini zinauhusiano wa karibu, na ipo haja yakuwashirikisha wanchi wa nchi hizi kwa karibu zaidi.
Katika mkutano huo, utaudhuliwa pia na rais wa Brazil, Lula da Silva, ambaye ndiye mwanzilishi wa ushirikiano wa karibu kati ya mabara haya.
Picha hapo juu, anaonekana rais wa Venezuela, Hugo Chavez , mmoja ya viongozi ambaye anaudhulia mkutano huo.

No comments: