Tuesday, June 9, 2009

Familia ya, Ken Saro Wiwa, na wenzake walipwa madai yao.

Mbrazili nyota asajiliwa kwa kitita kinene. Madrid, Uispania - 09/06/09.Timu ya Real Madrid,imemsajili mchezaji nyota wa Brazil, Kaka, kwa kitita cha $ 94.05million na kuvunja rekodi ya dunia. Kaka, ambaye alikuwa mchezaji wa, AC Milan, amevunja rekodi ya iliyo wekwa na, Zinedin Zidane, aliposajiliwa na mwaka 2001. Hata kwa mujibu wa wachunguzi wa maswala ya soka, wanasema bado Zinedine Zidane, anaweka rekodi ya kuwa mchezaji aliye nunuliwa kwa Euro 73million na Kaka Euoro 63, kwa kuzingatia mzunguko wa mabadiliko ya pesa ( Fedha). Picha hapo juu anaonekana, Kaka , akiongea na waandishi wa habari, muda baada ya kumaliza kufanya uangalizi wa afya mapema jana. Jose Emanuel Barroso,achaguliwa tena kuwa rais wa Muungano wa Ulaya.

Brussel, Belgium - 09/06/09.Muungano wa Ulaya,umemchagua tena, Jose Emanuel Barroso, kwa mara nyingine kuwa rais wa muungano huo kwa kipindi kingine cha miaaka mitano.
Akiongea baada ya kuchaguliwa kwake, kuendela kuwa rais wa muungano wa Ulaya, Jose Emanuel Barroso, alisema yakuwa imekuwa ni heshima kubwa kwake kwa kuchaguliwa tena kuwa rais wa muungano huo, na kuhaidi yakuwa atajitaidi kwa kila njia kuhakikisha muungano wa Ulaya utazidi kuwa imara.
Picha ya hapo juu, ni ya Jose Emanuel Barroso,ambaye amechaguliwa tena kuwa rais wa muungano wa Ulaya kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Picha ya pili, ni ya bendera ya muungano ya Ulaya,ambao umekuwa ukizidi kuwa imara kila kukicha.
Familia ya Ken Saro Wiwa na wenzake walipwa madai yao.
Niger Delta, Nigeria - 09/06/09.Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu nchini Nigeria, wataendelea kusukuma na kusisitiza kutaka kupata haki na ukweli kuhusu kifo cha aliyekuwa kiongozi wa kuteteta mazingira, Ken Saro Wiwa, aliye uwawa mwaka 10/11/1995, licha ya kampuni ya Shell kukubali kulipa malipo ya dola za Kimarekani 15.5 million kwa familia zilizopinga kuwepo kwa Shell katika jimbo la, Niger Delta, kwa madai ya kuchafua mazingira.
Hata hivyo, kampuni ya Shell, imekuwa ikikana kuhusika na sakata hilo lililo sababisha vifo vya Ken Saro Wiwa, na wenzake wengine wanane.
Picha hapo juu, ni picha ya kuchorwa ya, Ken Saro Wiwa, ambaye alikuwa kiongozi wa wanaharakati walio pinga kuwepo kwa Shell katika eneo la Niger Delta.
Picha ya pili, ni ya maeneo ambayo mfuta huwa yanahifadhiwa tayari kwa kusafirishwa.

No comments: