Sunday, October 3, 2010

Mashindano ya Jumuia ya Madola ya funguliwa.

Mashindano ya Jumuia ya Madola ya funguliwa. New Dheli, India - 03/10/2010. Wananchi wa India wamewakaribisha wanamichezo mbalimbali ili kushiriki mashindano ya nchi wanachama wa jumuia ya nchi zilizo kuwa koloni la Uingereza ambayo yanajulikana kama mashindano ya nchi za jumuia ya madola. Mashindano hayo ya 19th yameanza rasmi baada ya habari za wasiwasi kuenea ya kuwa itakuwa vigumu kwa mashindano hayo kufanyika kutoakana na maandalizi yaliyo tiliwa mashaka. Picha hapo juu wanaoneka wanamichezo wakishiriki wakati wa ufunguzi huku wakiongozwa na maonyesho yalioandaliwa kwa ajili ya ufunguzi.

Wajerumani kushangilia kumbukumbu ya muungano.
Berlin, Ujeruman - 03/10/2010.Wananchi wa Ujerumani wameshangilia siku ya kuungana Ujerumani ya Mashariki na Ujerumani ya Magharibi ambapo ziliungana 1990.
Muungano huo ulipokelewa kwa shangwe na wananchi wa Ujerumani na Ulaya kwa ujumla na umekuwa ukikumbukwa na kusherekewa kila mwaka.
Picha hapo juu anaonekana Kanselar wa Ujerumani Angela Merkel na viongozi wengine wakiangali kwa pamoja mazingira mapya baada ya muungano huo kutokea miaka 20 iliyo pita
China kuisaidia Greek kuinua Uchumi wake.
Athens, Greece - 03/10/2010. Serikali ya China imesema itaisaidia kikamilifu serikali ya Greek katika kujenga uchumi wake uliyo yumba.
Waziri mkuu wa China Wen Jiabao alisema " China itashiriki kikamilifu katika kuisaidia Greek kujijenga upya kiuchumi ili kupunguza deni ambalo ni mzigo kwa serikali kwa kuongeza ushirikiano wa karibu na kukuza biashara kati ya nchi hizi mbil."
Picha hapo juu ni ya bendera za China nchi ambayo itashirikiana kikamilifu na serikali ya Greek ili kuinua uchumi wa nchi hiyo.
Na picha inayo fuata chini ni ya Greek nchi ambayo inakabiliwa na tatizo la kiuchumi na kwa sasa itashirikiana na China kikamilifu ili kuinia uchumi wake.

No comments: