Friday, October 15, 2010

Venezuela ya saini mkataba na Urussi kujenga mitambo ya nguvu za kinyuklia.

Michezo ya 19 ya jumuia ya Madola yamalizika nchini India.

New Delhi, India 15/10/2010. Mashindano ya 19 ya nchi za jumuia ya Madola yamemalizika rasmi leo nchini India.
Katika mashindano hayo Australia ambayo imeondoka na medali nyingi za dhahabu zipatazo 74, ikifatiwa na Uingereza.
Akiongea wakati wa kufunga mashindano hayo rais wa michezo hiyo Mike Fennell alisema "michezo yote imekwisha vizuri na kila aliyeshiriki alifurahi japo kulikuwa na matatizo ya hapa na pale."
Picha hapo juu anaonekana mmoja ya watumbijazi akifanya vitu vyake wakati wa kufunga mashindano ya nchi ya jumuia ya Madola ya liyo fanyika nchini India
Picha ya pili wanaonekana washiriki na wanamichezo walioshiriki mashindano ya nchi wanachama wa jumuia ya Madola wakiwa uwanjani tayari kwa ufungaji wa michezo ya hiyo.
Venezuela ya saini mkataba na Urussi kujenga mitambo ya nguvu za kinyuklia
Moscow, Urussi - 15/10/2010.Serikali ya Venezuela imetiliana sahii mkataba na serikali ya Urussi kujenga mtambo wa nguvu za kinyuklia nchini Venezuela.
Mkataba huo uilisainiwa na waziri wa mambo ya nje wa Venezuela Nikolaus Maduro na rais wa mambo ya kinyuklia wa Urussi Sergie Kiriyenko.
Makataba huo kati ya serikali ya Urussi na Venezuela ulishuhudiwa na viongozi wa serikali zote mbili Hugo Chavez wa Venezuela na Dmitry Medvedev.
Mara ya kusaini mkataba, rais wa Urusi alisema "Venezuela ni mshiriki mkubwa wa Urussi katika nyanja za kimaendeleo."
Picha hapo juu anaonekana rais wa Venezuela Hugo Chavez kushoto akiwa na rais wa Urussi Dmitry Medvedev kulia mara baada ya kumaliza mazungumzo ya kiserikali.
Barabara ndefu duniani ya kamilika kuchimbwa
Milima ya Alps , Uswis 15/10/2010. Uchimbaji wa barabara chini ya milima ya Alps ambayo itakuwa barabara ndefu duniani kupita ndani ya mlima imemalizika.
Uchimbaji huo amabo ulianza miaka 15 iliyopita ulimalizika leo kwa kuunganisha barabara hiyo na barabara ambayo iliyopo Gottard Base.
Barabara hiyo itaunganisha kusini na kaskazini mwa Ulaya kiusafiri hasa ule wa mizigo mikubwa.
Picha hapo juu anaonekana mmoja ya wafanyakazi akiwa kazini kuanza ujenzi wa reli itakayo tumika kubebea mizigo.

No comments: