Tuesday, November 22, 2011

Luis Moreno-Ocampo awasili nchini Libya kwa mazungumzo.

Luis Moreno-Ocampo awasili nchini Libya kwa mazungumzo.

Benghazi, Libya - 22/11/2011. Mwanasheria mkuu wa koti ya kimataifa inayo husika na makosa ya ukiukwaji wa haki za binadamu amewasili nchi Libya ili kujadili na viongozi wa serikali ya mpito ni kwa jinsi gani kesi ya mtoto wa Muammar Gaddafi itaendeshwa.
Mwanasheria huyo Luis Moreno Ocampo alisema "huu ni mwanzo na wale wote ambao walio tenda makosa wafikishwe mbele ya vyombo vya sheria."
Luis Moreno Ocampo amewasili na msaaidizi wake Fatou Bensouda nchini Libya, huku serikalli ya mpito ikitaka kesi zidi Saif al-Islaam Gaddafi ifanyike nchini Libya, jambo ambalo mashirika ya kutetea haki za binadamu yanaa dai ya kuwa "hakutakuwa na haki katika kuendesha kesi, kwa kuzingatia mazingira yaliyopo."
Hata hivyo serikali ya mpito imesema "Saif al-Islaam atapata kila msaada katika kusikiliza kesi yake."
Saif al Islaam alikamatwa wakati akikimbia kutoka nje ya Libya hivi karibuni.

No comments: