Jeshi la Ethiopia ladaiwa kuingia nchini Somalia.
Gurel, Somalia - 20/11/2011. Wanajeshi wa Ethiopia wameonekana wakiingia nchini Somalia kwa kutumia Maroli na baadhi ya magari ya kijeshi.
Mzee mmoja wa kijiji Abdi Ibrahim alisema "nimeona magari ya kijeshi na maroli yakiwa yamebeba wanajeshi wa Ethiopia kuelekea eneo linaloshikiliwa na Shebab lililopo Galgudud."
Hata hivyo serikali ya Ethiopia imekanusha uvumi huo.
Kuonekana huko kwa wanajeshi wa Ethiopia nchini Somalia kumekuja baada ya jeshi hilo kuivamia Somalia mwaka 2006 kwa masaada wa Marakani na baadaye kujitoa kwa kushindwa kuleta amani nchini Somali.
Rais wa Syria asema yupo tayari kufa kutetea nchi yake.

Dumascus, Syria - 20/11/2011. Rais wa Syria amehaidi kupambana na wale wote ambao wanavuruga amaani nchini Syria baada ya makao makuu ya chama tawala kushambuliwa na mabomu.
Rais Bashar al Assad alisema " nipo tayari kufa kwa ajili ya nchi yangu, na nitahakikisha ya kuwa wale wote wanao vuruga amani wamekamatwa na ikiwa tutashambuliwa na jeshi lolote kutika nje basi itakuwa hali ya kutisha katika eneo zima la nchi za Kiarabu."
"ajisikia vibaya saana napo ona damu za watu wa Syria zinamwagika kwa sababu ya kundi fulani ambalo linavuruga amani, hivyo nilazima sheria zifuatwe ili kuweza kuleta amani nchini Syiria."
Na uamuzi wa nchi za jumuiya ya Kiarabu kuisimamisha Syria uanachama ni moja yaa nchi ya kuidhinisha uvamizi wa kijeshi ambao utaleta maafa makubwa." alisema rais Bashar Assad.
Nazo serikali za Uturuki naa Marekani zimebashiri ya kuwa huenda kukawa na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchi Syria na huku Urussi ikisisitiza kuwepo na mazungumzo ya amani yaanze mara moja.
Kundi la FARC lapata kiongozi mpya.

Bogota, Kolombia -20/11/2011. Kundi la FARC linalo pingana na serikali ya Kolombia limetangaza jina la kiongozi mwingine baada ya kiongozi wao mkuu wazamani Alfonso Cano kuuwawa na jeshi la Kolombia.
Timoleo Jimenez 52 amechaguliwa kushika madara hayo kufuatia kuwawa kwa Alfonso Cano mapema mwezi wa November mwaka 2011.
Wakitangaza FARC walisema " Komredi Timoleo Jiminez amechaguliwa kwa hali moja kuwa kiongozi wa FARC."
Mkuu huyo mpya wa FARC alipata mafunzo ya kijeshi nchini Kuba na Urussi naa amekuwa katika kundi la FARC tangu 1970.
Kundi la FARC limekuwa likipigana na serikali ya Kolombia inatosaidiwa na Marekani na inaaminika FARC inawapiganaji wapato 20,000.
Alqaida wadai kufaidika na vita vya Libya.

Algers, Algeria - 20/11/2011. Kiongozi wa kundi la Alqaida lililopo kaskazini mwa Afrika ameliambia gazeti moja la Nouakchott lililopo Mauritania ya kuwa kundi lake limefaidika kutokana na kuangushwa kwa serikali ya Muammar Gaddafi.
Mokhtar Belmokhtar aalisema " tumefaidika kwa kupata siraha nyingi ambazo zilikuwa zimefichwa na serikali ya Muammar Gaddafi na kundi letu litazidi kuimarika."
Tangu kuangushwa kwa Muammar Gaddafi, serikali za Magharibi zimekuwa na wasiwasi huenda baadhi ya siraha zimeangukia kwenye mikono ya kundi la Alqaeda na kuitaka serikali ya mpito ya Libya kufanya kila juhudi kuzifuatilia siraha hizo.
Amani ya kisiasa bado kupatikana nchini Misri.

Kairo, Misri-20/11/2011. Hali ya wasiwasi imezidi kuongezeaka nchini Misri, huku polisi wakiendelea kupambana na waandamanaji wanao pinga kuwepo kwa serikali ya kijeshi.
Polisi wakitumia mabomu ya kutoa machozi na risasi za mipira walikumbana na wakati mgumu wa kuwatawanya maaelfu ya watu waliokusanyika kwenye eneo lijulikananio kama Tahrir lililopo katikati ya jiji la Kairo.
Waandamanaji hao ambao walikuwa wakisema "hatutaki utwala wa kijeshi na Tantawi aondoke."
Kwa mujibu wa mmoja ya wafanyakazi wa huduma ya kwaza mtu mmoja alikufa hapo hapo baada ya kupigwa risasi ya plastiki na alikuwa anaitwa "Ahmed Mahmoud 23."
Waandamanaji hao wamekuwa wanatumia, fimbo, mbao na matofari ili kupamabana na polisi.
Misri imekuwa na myumbo wa amani tangu kuangushwa kwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Husni Mubbaraka mapema mwezi wa pili mwaka huu.
2 comments:
Hi to every one, as I am really eager of reading this blog's post to be updated daily. It contains good material.
Here is my homepage: loanluan []
ecig, e cigarette, electronic cigarettes reviews, smokeless cigarettes, smokeless cigarettes, smokeless cigarette
Post a Comment