Rais wa zamani wa Ivory Coast Laurent Gbagbo apelekwa Hague.

Hague Uhollanzi 29/11/2011. Aliyekuwa rais wa Ivory Coast na ambaye alitolewa madarakani kwa nguvu Laurent Gbagbo amewasilishwa jijini Hague tayari kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Lucie Bourthoumieux ambaye ni mwanasheria wa wa rais huyo alisema " Laurent Gbagbo amesha pekekwa nchini Uhollanzi."
Gbagbo alifunguliwa mashitaka na mahakama inayo husika na "utetezi wa haki za binadamu na makoso ya jinai."
Hata hivyo msemaji wa Gbagbo Abdon George Bayeto alisema " hii siyo haki kwa kitendo cha kumpeleka Laurent Gbagbo Hague kwani tukumbuke alishinda kwa 48% na hii italeta myumbo wa siasa na amani kuwa tete kati ya wa Ivory Coast."
Laurent Gbagbo alitolewa madarakani na kundi la chama cha mpinzani wake Alassane Ouwattara ambaye ndiye rais wa sasa wa Ivory Coast.
Mganga aliyekuwa akimtibu Michael Jackson afungwa miaka minne.


Los Angeles, Marekani - 29/11/2011. Mahakama jijini Los Angeles imemuhukumu mganga Conrad Murray 58 aliyekuwa mtabibu wa Michael Jackson jela miaka minne baada ya kukutwa na kosa la kuua bila kukusudia.
Akitoa hukumu hiyo Jaji Michael Pastor alisema " Conrad alikuwa na wajibu wa kufatilia maadili ya kitabibu lakini hakufanya hivyo na hukumu hii ina mstahili kutokana na kosa hili."
Mganga Conrad Murray alikutwa na kosa hilo wiki tatu zilizo pita baada ya kesi hiyo kusikilizwa kwa zaidi ya wiki sita
Aliyefanya mauaji ya kutisha nchini Norway adaiwa kuwa anaugonjwa wa Akili

Oslo, Norway - 29/11/2011. Mahakama inayo shughulikia kesi zidi ya muuaji aliye uawa watu 77 nchini Norway imeamua awekewe mtu wa kuchunguza ugonjwa wa akili.
Uamuzi huo umekuja baada ya mwanasheria kutoa ripoti ya kuwa Anders Behring Breivik anaugonjwa wa akili na hivyo apelekwe kwenye nyumba inayo shughulikia wagonjwa wa akili ili kutazamwa zaidi.
Anders alifanya mauaji makubwa nchini Norway mwezi wa saba, wakati alipo kwenda kuwashambulia vijana waliokuwa kwenye mkutano wa chama cha Labour cha inchi hiyo.
Wanafunzi wavamia ofisi za Ubalozi wa Uingereza nchini Iran.

Tehran, Iran - 29/11/20. Kikundi cha wanafunzi vijana nchini Iran wamevaamia ofisi za ubaalozi wa Uingereza na kuchoma bendara na kuharibu maeneo na mafaili ya kiofisi.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema " waandamanaji hao walitumia mabomu ya petrol, na kuchoma moto baadhi ya makaratasi ya kiofisi na huku wafanyakazi wa ofisi hiyo ya kibalozi ya Uingereza wakikimbia kuokoa maaisha yao."
Vijana hao walikuwa walisikika wa kisema "kifo kwa Uingereza, Izrael na Marekani na washiriki wake."
Serikali ya Uingereza imelaani kitendo hicho.
Hata hivyo polisi walifanikwa kuwatawanya vijana hao na kuhakikisha wafanyakazi waliokuwepo ndani ya jengo la ofisi hiyo ya kibalozi wapo salama.
Mahakama nchini Malasyia yawakuta na makosa Tony Blair na George Bush.


Kuala Lumpur, Malaysia 29/11/2011. Mahakama inayo shughulikia makosa ya kivita na ukiukwaji wa haki za binadamu iliyopo nchini Malaysia imewakuta waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair na aliye kuwa rais wa Marekani George Bush.
Kesi hiyo iliyo sikilizwa kwa muda wa siku nne kuanzia 19-22 Novemba kwenye mahakama ya Kuala Lumpur-The Kuala Lumpur War Crimes Tribunal or KLWCT, ilitoa uamuzi wake huo baada ya kusikilizwa kwa kesi hiyo iliyo letwa na wanasheria Gurdeal Singh Nijar na Francis Boyle, kwa kusema " tumewakuta na hatia Tony Blair na George Bush kwa kosa la kuondoa amani na kusababisha mauaji kutokana na vita vya Irak."
Hata hivyo katika kesi hiyo watuhumiwa hawakuweza kuwepo, ijapokuwa "mahaka imedai yakuwa watuhumiwa walipewa nafasi yakujitetea lakini hawakutokea wala kutuma wawakilishi wao."
Akiongea baada ya hukumu hiyo, mwanaharakati anaye pinga vita Mahathir Mohamed alisema " juhudi za mahakama zinazidi kuonekana na kukua ili kupambana na muundo mbinu wa kivita ambao umekuwa ukitumika vibaya na tutaendelea kupambana."
Mahakama hiyo ya Kuala Lumpur, imekuwa ikivilaumu vyombo vingine vya sheria kwa kushindwa kutekeleza sheria zinavyo sema, na kusababisha mashaka zidi ya jamii.
Kenya yatoa kibali cha kukamatwa rais wa Sudani.


Nairobi, Kenya - 29/11/2011. Serikali ya Kenya imetoa kibali cha rais wa Sudani kukamatwa pindopo atakanyaga nchini humo tena.
Akitoa kitambulisho hicho Jaji Nicolas Ombija alisema " rais Omar al Bashir atakamtwa ikiwa atakanyaga mguu wake nchini Kenya, kwani anahitajiwa na mahakama ya kimataifa iliyopo nchini uhollanzi ili kujibu mashitaka yanayo mkabili ya ukiukwaji wa haki za binadamu."
Uamuzi huo wa kutoa kibali cha kukamatwa kwa rais wa Sudan Omar al Bashir umekuja baada ya mahakama ya kutetea haki za binadamu iliyopo nchi Uhollanzi, kuilaaumu serikali ya Kenya kw kushindwa kumkamata rais huyo wa Sudani wakati alipo tombelea Kenya mwezi wa nane 2010.
1 comment:
Magnificent goods from you, man. I've bear in mind your stuff prior to and you're simply extremely
magnificent. I actually like what you've obtained here, really like what you're stating and the
way through which you assert it. You are making it enjoyable and you still care for to stay it smart.
I can't wait to learn much more from you. This is actually a wonderful web site.
Feel free to visit my homepage get targeted twitter followers
Post a Comment