Uispania yapata waziri mkuu mpya.
Madrid, Uispania - 21/11/2011. Chama chenye maadili ya mrengo wa kulia kimeshinda uchaguzi nchi Uispania.
Chama hicho People Party -PP, kimefanikiwa kupata viti kwa wingi kuliko vyama vingine vyenye idadi ya 186 kati ya 350 katika bunge.
Akihutubia baada ya ushindi huo, kiongozi wa chama hicho Mariano Rajoy 56, alisema " bado kuna wakati mgumu wa kuinua uchumi na hakutakuwa na maajabu na hivyo hakuna haja ya kuhaidi, na tutafanya kila njia kutatua matatizo yaliyopo."
Spain nchi ambayo inamatatizo makubwa ya ukosefu wa kazi, na zaidi ya million tano ya watu hawana kazi, wangi wao wenye umri kati ya miaka 25-46
Viongozi wa upinzani wa serikali ya Syria wakutana na serikali ya Uingreza.

London, Uingereza - 21/11/2011. Viongozi wapinzani wa serikali ya Syria wamekutana waziri wa mambo ya nchi za nje wa Uingereza ili kujadili hali halisi ya kisiasa iliyopo nchini Syria.
Viongozi hao wa upinzani wamekuta na serikali ya Uingereza ili kuishinikiza serikaali ya rais Bashar al Assad, ili alete mabadiliko ya kisiasa nchini Syria.
Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza William Hague alisema "Rais Assad lazima aelewe ya kuwa viongozi wa serikali ya upinzani wanatambulika na wapo tayari kuleta mageuzi."
Na utawala wa Assad utazidi kuwa na wakati mgumu kwani serikali nyingi zipo tayari kufanya kazi na viongozi wa upinzani." alimaliza waziri Hague.
Katika mazungumzo hayo, waziri wa mambo ya nchi za nje wa Syria, aliwataka viongozi hao waige mfano wa viongozi wa upinzani wa Libya walioungana kumng'oa Muammar Gaddafi.
Syria imekumbwa na maandamano ambapo wananchi wanadai mabadiliko ya siasa lazima yafanyike na rais Assad ajitoe katika maadaraka.
Maandamano yafanya waziri mkuu kujiudhuru.

Kairo. Misri - 21/11/2011. Waziri mkuu anayeliongoza baraza la mawaziri wa serikali ya mpito wa Misri ameandika barua ya kujiudhuru kutokana na maamndamano yanayo endelea nchi humo.
Essam Sharaf aliandika barua hiyo na kuikabidhisha kwa kamati ya kijeshi ya nchi hiyo kufuatia mauaji ya watu 33 yaliyo tokea baada ya polisi na wanajeshi kupigina na waandamanaji wakati wa kutuliza ghasia.
Habari kutoka ofisi ya wizara ya afya zinasema " watu wapatao 33 wameuwawa na 1,500 kujeruhiwa tangu maandamano hayo yaanze hivi karibu."
Maandamano haya ambayo nimakubwa tangu kuangushwa kwa rais Husni Mubaraka, yaliitishwa ili kuishinikiza serikali kufanya mabadiliko ya kisiasa haraka.
Kufuatia kujiudhuru huko kwa waziri mkuu ssam Sharaf, wasiwasi mkubwa umetanda nchi humo, kwani ni siku chache zimebakia kabla ya uchaguzi wa bunge kuanza.
1 comment:
fantastic put up, very informative. I'm wondering why the other specialists of this sector do not realize this. You should proceed your writing. I am confident, you have a great readers' base already!
my homepage :: logjamming ()
Post a Comment