Wednesday, November 16, 2011

Mario Monti aapishwa kuwa waziri kuwa mkuu wa Itali.

Mario Monti aapishwa kuwa waziri mkuu wa Itali.

Roma, Itali - 16/11/2011. Mario Monti ameapishwa kuwa waziri mkuu wa Itali, siku chache baada Silvio Beruscon kujiudhulu.
Mario Monti ambaye alishawahi kuwa kamishna katika jumuiya ya Ulaya.
Baada ya kuapishwa waziri mkuu Monti aliunda baraza la mawaziri tayari kuandaa mkakati wa kupambana naamyumbo wa uchumi uliyoikumba Itali.
Jumuiya ya nchi za Kiarabu yatoa onyo kwa Syria.
Rabat, Morokko - 16/11/2011. Jumuiya ya nchi za Kiarabu imetoa siku tatu kwa nchhi ya Syria kusimamisha vurugu zinazotokea kati ya serikali na wapinzani au hatua nyingine zitachukuliwa.
Msemaji wa katika mkutano huo alisema " tunataka serikali ya Syria kusimamisha umwagaji wa damu unao endelea na ukandamizwaji kwa wapinzani usimamishwe."
Onyo hilo limetolewa baada ya jumuiya hiyo kuiwekea vikwazo serikali ya Syria hivi karibuni.

No comments: