Mtoto wa Muammar Gaddafi akamatwa.

Obari, Libya - 19/11/2011. Mtoto wa aliye kuwa kiongozi wa Libya Muammar Gaddafi amekamatwa katika mji wa Obari uliyopo kusini mwa nchi hiyo.
Saif al-Islam, ambaye alikuwa mafichoni tangu serikali ya baba yake kuangusha na kuwawa na kundi la National Transitional Council (NTC) chini ya msaada wa jeshi la NATO mapema mwezi wa kumi 2011.
Waziri wa sheria wa Libya Mohammed al Allagui alisema "Saif atawasilishwa Tripol."
Hata hivyo, kiongozi aliye ongozwa kukamatwa kwa Saif alisema " Tutamweka hapa Zintan hadi hapo serikali itakapo undwa na ndiyo hapo tutamkabidhi mikononi mwa serikali."
Saif al-Islam amesha funguliwa kesi na mahakama ya kimataifa inayo shughulikia makosa ya kibinadamu iliyopo nchini Uhollanzi ili kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Papa Benedikt awasili nchini Benin.

Benin, Katounou - 19/11/2011. Papa Benedikt XVI amewasiili nchini Benin kwa mara ya pili huku maelfu ya wananchi wakimshangilia kwa shwangwe.
Msemaji wa ofisi ya Vatikani alisema "katika ziara yake Pope Benedikt, atatembelea sehemu tofauti na kusisitiza umoja na ushirikiano ili kukuza amani hasa katika bara la Afrika, huenda akakutana na wakati mgumu wa kujibu maswali juu ya matumizi ya kondom."
Nchi ya Benin ambayo waumini wa kanisa Katoliki wanazidi kuongezeka tangu kuwasili kwa mapadri wa Kikatoliki miaka 150 iliyo pita kuanzisha seminari kubwa ya kikatoliki katika eneo la Afrika ya Magharibi.
Vatikan yakasirishwa na picha zilizo chapishwa zidi ya kiongozi wa kanisa Katoliki.

Vatican, Vatican City -19/11/2011. Kanisa Katoliki limelaani kitendo cha wanakampeni zidi ya ushoga kuchapisha picha za kiongozi wa kanisa hilo akipigana busu na kiongozi mmoja wa dini ya kiislaam.
Habari kutoka kanisa hili zimesema "picha hizo lazima ziziuliwe na kuwekwe sheria kuzuia picha kama hizo."
Picha hizo za Papa Benedikt akibususiana na kiongozi mwingine wa dini, ni moja ya picha ambazo zimesambazwa na kuonyeshwa ni za waziri mkuu wa Izrael Benyamini Netanyahu akimbusu rais wa Wapalestina Mahamoud Abbas, na huku rais Sarkoz akibusiana na Kansela Angel Markel wa Ujerumani.
Meya akutwa nahatia ya kuhusika na mauaji ya kimbali na ahukumiwa kwenda jela.
Kigali, Rwanda - 19/11/2011. Mahakama ya kimataifa inayo shughulikia haki za binadamu iliyopo nchini Rwanda imemuhukumu aliyekuwa meya wa mji wa Kivuma kwa kuhusika katika mauaji ya kimbali yaliyo tokea mwaka 1994.
Gregoire Ndahimana ambaye alikutwa na makosa ya kusaidia " mauaji ya watu wasio pungua 4,000 wenye asili ya Kitutsi."
Kwa mujibu wa mahakama "Ndahimana alikuwepo kama kiongozi wa serikali wakati wa mauaji yaliyo tokea katika kanisa Katoliki lililopo Nyange."
Gregoire Ndahimana atatumikia kifungo cha miaka 15 jela, japo kwa sasa ameshatumikia miaka miwili kutokana yanayo husika na maswala ya mauaji ya kimbali yaliyo tokea Rwanda 1994.
No comments:
Post a Comment