Zuriki, Uswizi - 01/06/2011. Wajumbe wa shirikisho la soka duniani FIFA,wamemchagua tena rais wa shirikisho hilo kushikiria kiti hicho kwa kipindi kingine cha miaka minne.
Wajumbe hao waliweza kumchagua Sepp Blatter kwa wingi wa kura zipatazo 186 kati ya kura 203 zilizo pigwa.
Sepp Blatter, ambaye alikuwa mgombea pekee katika kiti hicho, baada ya mpinzani wake Mohamed bin Hammam kujitoa kutokana na kashfa za rushwa.
Hata hivyo, uchaguzi huo ulifanyika baada ya Uingereza kushindwa kuwashawishi nchi wanachama wa shirikisho hilo kupiga kura ya kutaka uchaguzi huo usimamishwe kwa muda, ili achaguliwe mpinzani dhidi ya Sepp Blatter, lakini matokea ya kura hizo yalipinga maombi ya Uingereza kwa 172 kutaka uchaguzi ufanyike na 17 kuunga mkono Uingereza.
Kuchaguliwa kwa Sepp Blatter, kumeaandamana na misukosuko mingi iliyo ikuta shirikosho hilo baada ya kashfa za rushwa kuandama uongozi mzima wa shirikisho hilo FIFA.
Akiongea baada ya matokeo ya uchaguzi, rais huyo wa FIFA Sepp Blatter alisema "Mimi ni kaptain ambaye naongoza jahazi lililo kumbwa na mawimbi na tuta hakikisha shirikisho la soka litakuwa mairi na kulinda heshima ya mchezo huu, kuweka wazi kila jambo na kuhakikisha matatizo yaliyo tokea hayatotokea tena, na nahaidi kwa baraka za Muumba na uzima atakao nipa basi tuta fanikiwa kuhakikisha shirikisho hili lina kuwa swafi na imara."
Mtuhumiwa wa mauaji ya Bosnia Serbi Ratko Mladik awasilishwa Hague kujibu mashitaka.
Hague, Uhollanzi -01/06/2011.Aliyekuwa mkuu wa majeshi wa Bosnia Serbia ambaye anashutumiwa kwa kuhusika na mauaji yaliyo tokea wakati wa vita 1992-95 nchini humo amewasilishwa kwenye mahakama ya kutetea haki za binadamu ili kujibu mashitaka yanayo mkabili.
Ratko Maladik, atafikishwa mahakamani siku ya Ijumaa tayari kuanza kusikiliza kesi yake itakayo endeshwa jaji kutoka Uhollanzi.
Kwa mujibu wa habari kutoka mahamani zinasema "Mladik anakabiliwa kujibu mshitaka yaziyo pungua 11."
Ratko Mladik, alikamatwa baada ya kukumbia mafichano kwa muda usiyo pungua miaka 16 iliyo pita.
Hussein Mubaraka na watoto wake wawili kufikishwa mahakamani.
Kairo, Misri 01/06/2011. Serikali ya Misri imetangaza ya kuwa aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo atafikishwa mahakamani yeye na watoto wake kujibu mashitaka ya kusababisha maafa yaliyo tokea wakati wa maandamano ya kutaka ang'olewe madarakani kwa rais huyo.
Kwa mujibu wa habari kutoka serikali zinasema " Hussein Mubaraka na watoto wake wawili wa kiume watafikishwa mahakamani kuanzia tarehe 13, mwezi wa nane."
Habari hizo pia zilisisitiza yakuwa ikiwa "Hussein Mubaraka atakutwa na hatia ya kuhusika na machafuko yaliyo sababisha mauaji wakati wa kutaka atolewe madarakani baada ya kutawala Misri kwa muda wa miaka 30, basi huenda akaukumiwa adhabu ya kifo."
Rais Hussein Mubaraka alitolewa madarakani baada ya maandamano yaliyo chukua siku 18 ya kutaka atoke madarakani.