Al-Qaida wamteua Ayman al Zawahri kuwa kiongozi mkuu.


Ayman al Zawahri ameteuliwa rasmi baada ya majadiliano yaliyo chukua wiki sita tangu kuuwawa kwa kiongozi wa Al-Qaida Osama bin Laden na jeshi la Amerika nchi Pakistan.
Akiongea baada ya uteuzi huku bunduki ikiwa pembeni yake, Ayman al Zawahri alisema " tutaendelea mapmbano yetu kama kawida na kuonya ya kuwa wale Amerika itakumbana na upinzani ambao hapo mwazo haukuwepo."
Ayman al Zawahri ambaye ni rai wa Misri alijiunga na Al-Qaida mwaka 1986 baada ya kukutana na aliye kuwa kiongozi wa kundi hilo hayati Osama bin Laden katika mji wa Peshawar nchini Pakistan.
Kiongozi wa aliyeshukiwa kuongoza mauaji ya Bali afungwa.

Jakarta, Indonesia - 16/06/2011. Mahakama kuu jijini Jakarta imemuhukumu aliyekuwa mkuu wa kundi la Jemaah Islamia kwa kosa lakuwafadhili wapiganaji wa kundi la Aceh wanaopingana na serikali ya Indonesia.
Abu Bakar Bashir, ambaye amehukumiwa kifungo cha miaka 15 baada ya kukutwa ya kuwasaidia wapinzani wa serikali wa kundi la Aceh, ambao wao walitaka kumwua rais .
Wakati wa hukumu hiyo, polisi na wana usalama walikuwa makini ili kuzua machafuko ambayo yangeweza kutokea kwenye maeneo ya mahakama hiyo.
Abu Bakar Bashir, anashutumiwa pia kwa kuhusika katika milipuko ya bomu iliyo tokea Bali mwaka 2002 na kusababisha mauaji ya watu wasiopungua 200 wengiwao wakiwa watalii.
Nokia yashinda kesi zidi ya Appple.

Ushindi huo umekuja baada ya kesi iliyo funguliwa na Nokia mwaka 2009,kwa madai Apple imekuwa ikitumia baadhi ya teknolojia zake.
Akiongea mara baada ya kupata ushindi wa kisheria, mkurugenzi mkuu wa Nokia Stephen Elop, alisema " tunafurahi kuona sas Apple wamejumuika katika kutumia teknologia za Nokia na hii ni mwanzo wa na sisi wote tunaweza kuundelea na biashara bila matatizo."
Hata hivyo malipo ambayo yanatakiwa yalipwe na Apple,hayakuweza kupatikana kutokana na makubaliano yaliyo wekwa kati ya mashirika hayo mawili.
No comments:
Post a Comment