Tuesday, June 28, 2011

Waziri wa fedha wa Ufaransa kuongoza -IMF- shirika la fedha.

Waziri wa fedha wa Ufaransa kuongoza -IMF- shirika la fedha.
New York, Marekani-28/06/2011. Shirika la kimataifa la fedha duniani IMF-International Monetary Fund, limemchagua waziri wa fedha wa Ufaransa kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika hilo ili kushika nafasi iliyo achwa na Dominique Strauss-Kahn ambaye amejiudhulu kutokana na kuwa na kesi ya kijinsia.
Christine Lagarde, amechaguliwa kushika nafasi hiyo na kuwa mwanamke wa kwanza kushika kiti cha oungozi wa shirika hilo.
Kuchaguliwa huko kwa waziri wa fedha wa Ufaransa kumefanikwa baada ya kuungwa mkono na Marekani.Rasi wa Ufaransa, Nicola Sarkozy alisema " nivizuri kwani shirika hilo limepata kiongozi mwanamke kwa mara ya kwanza na ambaye anauwezo wakimataifa."
Serikali ya Ugiriki yapambana na wanaopinga uamuzi.
Athensi, Uguriki- 28/06/2011. Maelfu ya Wagiriki wameaandamana kupinga uamuzi wa serikali kutaka kugeuza sheria za kiuchumi nchini humo.
Habari kutoka ndani ya serikali zinasema "serikali ya Ugiriki upo na wakati mgumu wa kupambana maandamano ya nayo endelea na kuamua ni kwa jinsi gani itaweza kutuliza hasira na upinzani ambao serikali hiyo inakumbana nazo kutoka na hatua ya serikali kutaka kubana matumizi na kugeuza baadhi ya sheria za kiuchumi."
Maandamano hayo ambayo yameongozwa na vyama vya wafanyakazi kulekea katikati ya jiji la Athensi kwenye eneo la Syntagma yalikumbana na nguvu za polisi na kuleta ghasi kubwa na kusababisha maafa makubwa ya kijamii na mazingira.

No comments: