Monday, June 27, 2011

Mahakama ya Hague yataka Muammar Gaddafi akamatwe.

Mahakama ya Hague yataka Muammar Gaddafi akamatwe.
Hague, Uhollanzi - 27/07/2011. Mahakama ya makosa ya jinai na kutetea haki za binadamu nchini Uhollanzi imetoa kibali maalumu cha kutaka kiongozi wa Libya, mtoto wake wa kiume na afisa mkuu wa usalama wa taifa wakamatwe.
Jaji wa Sanj Mmmasenono Monageng, alitangaza ruhusa hiyo kwa kusema " kutokana na ushahidi uliyo tolewa na mwanasheria mkuu wa mahakama hiyo ya kimataifa Louis Moreno-Ocampo zimeonyesha ushahidi wakutosha yakuwa kiongozi huyo wa Libya Muammar Gaddafi, mtoto wake Seif al Islam na afisa mkuu wa usalama wa taifa Abdullah Senussi wamahusika katika kukiuka haki za binadamu na hivvyo lazima wakamatwe."
Hata hivyo serikali ya Libya imesema haifanya makos hayo yanayodaiwa na makosa hayo ni ya jeshi la NATO.

No comments: