Thursday, June 23, 2011

Marekani na Washiriki wa NATO kuondoa wanajeshi nchini Afghanistan.

Marekani na Washiriki wa NATO kuondoa wanajeshi nchini Afghanistan.
Washington, Marekani-23/07/2011. Rais Baraka Obama wa Amerika ametangaza kuwa serikali ya Amerika wanajeshi wapatao 33,000 watarudi nyumbani kutoka Afghanistan ifikapo msimu wa kiangazi wa mwaka 2012.
Kufuatia kutangazwa huko kwa serikali ya Amerika kupunguza wanajeshi nchini Afghanistan, nchi washiriki wa NATO nazo zimeanza kutangaza mpango wa kutaka kuondoa wanajeshi zikiongozwa na Uingereza.
Kufuatia uamuzi wa nchi za NATO kuanza kuondoa majeshi yake nchini Afghanistan, rais wa nchi hiyo Hamid Karzai ameunga mkono uamuzi huo kwa kusema kuanza kuondoka kwa wanajeshi wa NATO ni mwanzo wa Waafghanistani kuanza kuchukua madaraka ya ulinzi na kuwa mikononi mwao."
Hata hivyo habari kutoka ndani ya bunge la Amerika zinasema, rais Obama,ametoa kwa wingi jeshi hilo nchini Afghanistan na hawafahamu yambele yatakayo tokea.
Rais Hugo Chavez afanyiwa matibabu nchini Kuba.
Havana, Kuba 23/06/2011. Rais wa Venezuela anaendela kupata nafuu baada ya kufanyiwa upasuaji kwa ajili ya matibabu.
Rais Hugo Chavez 56 alikwenda nchini Kuba baada ya kusumbuliwa na pelvic abscess Juni 10.
Habari kutoka ofisi ya rais zinasema " rais Hugo Chavez anatarajiwa kurudi kazini muda si mrefu na makamu rais Elias Jaua anaongoza ofisi kwa sasa."
Kwanda huko kwa ajili ya matibabu kwa rais wa Venezuela kumekuja kutoka na uhusiano wa karibu wa nchi hizo mbili, japo inaaminika ya kuwa Kuba hali ya kufanyia kazi ya matibabu ni duni.
Kesi zidi ya mwanasiasa na kiongozi maarufu nchi Uhollanzi yafutwa.
Amsterdam,
Uhollanzi 23/06/2011. Mahakama ya jiji la Amsterdam imefutilia mbali kesi zidi ya mwanasiasa na kiongozi wa chama cha uhuru, ambayo ilikuwa imefunguliwa zidi yake kwa kukashifu,kuchochea utenganifu na hasira katika jamii.
Geert Wilders, ambaye alishiriki katika picha iliyo itwa "Fitna" ambayo ilitolewa mwaka 2008, na kuleta mvutano mkubwa kwa kusema " dini kislaama haina nafasi katika mila za Ulaya," jambo ambalo lilisababisha waumini wa dini ya Kislaam kukasirika.
Akiongea katika hukumu hiyo hakimu alisema" maneno aliyo yaongea Geert Wilders kuhusu dini ya Kislaam siyo makosa kufuatia sheria za nchi na hakuleta madhara katika jamii."
Akiongea nje ya mahakama Wilders alisema "nipo hapa kwa sababu ya yale niliyo yasema, nitaendelea kusema na sitakaa kimya.
Kesi zidi ya mwanasiasa huyo iliaanza mwaka 2010.

No comments: