Sunday, June 12, 2011

Huwa nasoma Kuraan na Biblia asema Tony Blair.

Afrika ya Kusini ya muaaga mama wa ukombozi zidi ya Ubaguzi wa rangi.
Soweto, Afrika ya Kusini-13/06/2011. Wananchi wa Afrika ya Kusini wamekumbwa na huzuni na msiba mkubwa baada ya kuondokewa na mwanaukombozi na mama wa Afrika ya kusini aliye pigana kidete kupinga ubaguzi wa rangi.
Albertina Sisulu, ambaye alikuwa mke wa hayati Walter Sisulu 92 alifariki dunia nyumbani kwake jijini Johannesburg.
Watu wapatao 40,000 walikuwepo kwenye misa ya kumuuga hayaati Albertina iliyo fanyika kwenye uwanja wa mpira wa SOWETO.
Rais wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma, amesema "msiba wa kuondokewa Albertina ni wa kitaifa na takumbukwa kwa mchango wake wa kuung'oa ubaguzi wa rangi."
Nelson Mandela, ambaye alikuwa rais wa kwanza wa Afrika ya kusini baada ya kuung'oa ubaguzi wa rangi alisema katika waraka wale uliyo somwa na mke wane Graca, " Albetina ulikuwa sehemu ya maisha yangu wewe na mumeo Walter na nitawakumbuka milele na ningependa kuwepo kukuaga kwa mara ya mwisho na najaribu kufikiria ya kuwa Albertina anakwenda kutana na wapigania uhuru wenzake Oliver Tambo. Walter na Heren Joseph nakushukuru kwa yote tuliyo fanikwa niee salaamu zangu kwa mashujaa wenzangu." Mabida
Albertina Sisulu amepumzishwa karibu na hayati mume wake Walter Sisulu.
Huwa na soma Kuraan na Biblia asemaTony Blair.
London, Uingereza -12/06/2011. Aliyekuwa waziri mkuu wa zamani wa Uingereza amekubali ya kuwa miaka ya 70 dunia nzima ilikuwa haina mawazo ya kutosha kupambana na hali halisi na tangu kutoka madarakani ameweza kujua hali halisi kwa kusoma vitabu hasa vya dini.
Tony Blair aliseme " hali imekuwa ngumu kimaisha na ipo nia ya kuhakikisha yakuwa matajiri kuwasidia watu wasiona uwezo. Kwani itakuwa siyo haki kwa mtu mmoja kuwa na utajiri mwingi na wengi wanishi katika haki mbaya."
Akiongeza Tony Blair "kuwa na imani ni muhimu saana kwani kunakuwezesha kujua ukweli wa mabo yanayotokea duniani na huwa nasoma bibilia na Kuraani ambavyo vinanisaidia kuelewa kiundani hali halisi."
Tony Blair ambaye ni kiongozi anayesimamia kupunguza mgogoro uliyoko kati ya Izrael na Palestina amekubali pia tangu atoke madarakani amelewa kiundani hali halisi kati ya Wapalestina na Waizrael.

No comments: