Sunday, June 19, 2011

Mvutano wa siasa nchini Somalia, waziri mkuu ajitoa madaarani.

Mvutano wa siasa nchini Somalia, waziri mkuu ajitoa madaarani.
Mogadishu, Somalia-19/06/2011. Waziri mkuu wa Somalia ametangaza kujiudhulu baada ya kukubaliana na rais na spika wa bunge.
Waziri Mohamed Abdulahi Mohamed alisema " kufuatia mtazamo wangu kuhusu hali halisi ya nchi yetu na makubaliano yaliyowekwa Kampala Uganda na napenda kumshuruku rais na wanchi wenzangu kwa massada walionipa wakati wa uongozi wangu.
Mapema mwaka huu waziri mkuu wa huyo ambaye ailtakiwa kujihudhulu lakini alikataa kwa kutaka kuwepo na kura ya imani zidi yake.
Somalia nchi iliyopo kwenye pembe ya Afrika Mashariki imekuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu kuanguka kwa rais Mohamed Siad Barre mwaka 1991 na imekuwa ikizaniwa ya kuwa ni moja ya makazi ya kundi la Al Qaeda.
Mameya wa miji nchini Marekani wataka vita kusimamishwa.
Balttimore, Marekani - 19/06/2011. Mameya wa miji ya nchini Marekani wamekutana katika mji wa Baltimore na kulitaka bunge la nchi yao kupitisha mswada wa serikali kusimamisha vita nchini Afghanistan na Irak ambavyo vinaitia hasara taifa kifedha na kijamii.
Wakiongea katika hotuba ya pamoja ambayo ilisomwa na Elena Temple alisema " Mkutano mkuu wa Mameya wa Marekani unaliomba bunge la nchi kusimamisha vita na kuelekezea fedha zinazo tumika katika vita hivyo kwenya sekta za kijamii ili kuinua uchumi wa nchi."
Vita vinavyo endelea hadi sasa vimekuwa vikitumia zaidi ya mamillion kwa mwaka na kuleta maafa makubwa katika jamii.

1 comment:

Rizki al-haddad said...

http://adf.ly/584521/blead-hecker