Thursday, March 12, 2009

Aliyemrushia kiatu rais Bush ahukumiwa miaka 3 jela.

Ufaransa na Ujerumani kudumisha ushirikiano zaidi. Berlin, Ujerumani 12/03/09. Kansella wa Ujerumani, Angela Merkel, amempongeza rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy, kwa uamuzi wa nchi yake kurudi kikamilifu katika jumuia ya ulinzi ya NATO. Kansella,Angela Merkel, aliyasema haya, wakati alipo kutana na rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy, ambaye yupo ziarani nchini Ujerumani,ili kujadili ni jinsi gani nchi hizi mbili zitashirikiana zaidi. Picha hapo juu wanaonekana rais, wa Ufaransa,Nicolas Sarkozy, akikaribishwa mjini Berlini na Kansella, Angela Merkel mapema leo. Madaktari na muuguzi watekwa nyara Darfur. Darfur, Sudan-12/03/09.Waanyakazi watatu wa shirika la madakitari wa sio na mipaka wametekwa nyara na watu wasiojulikana. Wafanyakazi hao wanao tokea, Kanada na Itali, waliingiliwa katika ofisi zao zilizopo,Saraf Umra na kuchukuliwa kwa nguvu huku mitutu ya bunduki ikiwa nyuma yao. Kuafuatia hali ya usalama kuwa mbaya katika eneo hilo la Darfur, shirika hilo limeamua kuamishia ofisi zake mjini Kartoum. Picha hpo juu, linaonekna moja ya gari, lililo kuwa likitumiwa na ma wafanyakazi hao waliotekwa nyara mapema leo.

Aliye mrushia kiatu rais Bush, ahukumiwa miaka 3 jela.
Baghdad, Irak-12/03/09. Mwandishi wa habari Muntadher al Zaidi, aliyemrushia kiatu aliyekuwa rai wa Amerika George Bush, amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu.
Wana habari huyo, Muntadher al Zaidi,mwenye miaka 30, alihukumiwa baada ya kupatikana na hatia ya kumshambulia na kumdhalilisha kiongozi wa kigeni aliye tembelea nchi hiyo.
Hata hivyo, mwakili wa Muntadher al Zaidi, wamesema watakata rufaa, kufuatia hukumu hiyo.
Picha hapo juu wanaonekana, baadhi ya watu wakiandamana kuelekea mahakamani huku wamebeba picha za Muntadher al Zaidi.
Picha ya pili anaonekana, Muntadher al Zaidi,anaonekana akirusha kiatu wakati, rais George Bush alipo tembelea nchini Irak.
Picha hapo juu,

No comments: