Mke wa rais afungwa jela miaka mitatu.
Lusaka, Zambia - 03/03/09. Mke wa rais wa zamani wa Zambia Frederick Chiluba, amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu na nusu, baada ya kukutwa na hatia ya kupokea pesa kinyume cha sheria.
Ka mujibu wa mahakama,Bi Regina Chiluba,alipokea pesa hizo za serikali na kuzitumia kwa kujengea nyumba na kufanyia biashara wakati mume wake alipo kuwa rais.
Wakati wa hukumu hiyo, rais huyo wazamani wa Zambia, Frederick Chiluba, alikuwepo mahakani,
Hata hivyo rais huyo wa zamani wa Zambia, anakesi inayo mkabili kwa kutumia vibaya pesa za umma wakati akiwa madarakani.
Picha hapo juu wanonekna, rais wa zamani wa Zambia, Frederick Chiluba na mkewe bi Regina Chiluba, wakiwa mahakamani siku chache kabla ya hukumu ya kwenda kutumikia kifungo cha miaka kwa miaka mitatu na nusu kwa bi Regina Chiluba kutolewa leo 03/03/09.
Ulimwengu wa mchezo wa kriket waingia doa kubwa nchini Pakistan.
Lahore, Pakistan - 03/03/09.Wapakistan sita wamepoteza maisha yao na wachezaji sita wa timu ya Kriket ya Sri Lanka,kujeruhiwa vibaya baada ya watu wasiojulikana kushambulia msafara huo wa wachezaji karibu na uwanja wa Gaddafi, wakati tumu ya Pakistan ikicheza na Sri Lanka.
Washington, Amerika - 03/03/09.Waziri mku wa Uingereza , Gordn Brown, amefanya ziara rasmi nchini Amerika, kwa mazungumzo ya kiserikali.
Jerusalem,Izrael -03/03/09. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Bi, Hillary Clinton, amefanya mazungumzo viongozi wa Izrael,na kusisitiza yakuwa Amerika itashirikiana na Izrael kwa kila hali.
No comments:
Post a Comment