Tuesday, March 23, 2010

Baraka Obama atia saini muswada mpya wa bima ya afya kwa Waameika.

Baraka Obama atia saini muswada mpya bima ya afya kwa Waamerika.

Washington, Amerika - 23/03/2010. Rais wa Amerika amesaini muswada wa bima ya afya na kufanyiwa mabadiliko ambayo itawawezesha Waamerika wapatao million 32 watapata matibabu bila matatizo.
Rais Baraka Obama amesaini muswada huo kuwa sheria mbele ya baadhi ya wananchi na viongozi wa serikali.
Baraka Obama alisema " Nimesaini muswada kuwa sheria na afya ya kila mwananchi kila mwanchi wa Amerika itathaminiwa kwa usawa."
Picha hapo juu anaonekana rais Baraka Obama akisaini muswada wa wa bima ya afya kwa wote hivi karibuni.
Serikali ya Izrael kuendelea na ujenzi wake.
Washington, Amerika - 23/03/2010. Waziri mkuu wa Izrael ameliambia balaza la wa Izrael na Amerika ya kuwa serikali yake itaendelea na ujenzi wa nyumba na makazi kwa ajili ya watu wake.
Akiongea, waziri mkuu Benyamini Netanyahu alisema "kila mtu anajua, Amerika Ulaya na Wapalestina wanajua ya kuwa ujenzi wa makazi ni moja ya makubaliano ya kuleta amani." Na ujenzi wa Jerusalem ni sawa na ujenzi wa Telavivi, hivyo ujenzi hautazuia kuwepo kwa mataifa mawili ya Waizrael na Wapalestina."
Picha hao juu anaonekana, waziri mkuu wa Izrael Benyamin Netanyahu, akiongea na wajumbe wa AIPAC.
Uingereza ya mrudisha nyumbani balozi wa Izrael.
London, Uingereza - 23/03/2010 .Serikali ya Uingereza imemrudisha nyumbani mmoja wa balozi wa Izrael nchini Uingereza kutokana na mauaji ya kiongozi wa kundi la Hamas katika nchi za muungano wa nchi za Kiarau United Arab Emarate, (UAE).
Akiliambia bunge, waziri wa mambo ya nchi za nje David Miliband alisema "Tunayo sababu ya kuamini ya kuwa pasport za Uingereza zilitumika kusafiria kuingia na kutoka katika nchi za UAE."
"Kitendo hicho kimeishichia hadhi taifa."
Mvutano huo unakuja baada ya kuuwawa kwa kiiongozi wa HamasMahmoud al Mabhouh katika nchi za muungano wa Kiarabu na kuleta mgogoro wa kidlomasia.
Picha hapo juu ni ya waziri wa mambo ya nje wa Uingereza, ambaye ametangaza kurudishwa kwa balozi wa Izrael.

No comments: