Rwanda yarudisha madini ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Kigali, Rwanda - 03/11/2011. Serikali ya Rwanda imerudisha madini zaidi ya tani 82 yaliokamatwa na polisi nchini Rwanda na kurudishawa Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo.
Naibu mkurugenzi wa mali ya asili wa Rwanda " Michael Biryaberema alisema " Rwanda inataka kukomesha uchimbaji huo haramu na kufuta fira ya kuwa Rwanda inafaidika na kutokana na madini yanayo toka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Rwanda na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zitashirikiana kwa pamoja katika kuimarisha sekta ya madini."
Madini ambayo yamerudishwa ni pamoja na yale ya cassiterite, bati na vile vile coltan, ambayo hutumiwa kujenga vifaa kama vile simu za mkononi.
Kurejeshwa kwa madini hayo kunafuatia sheria za kimataifa zinazonuiwa kusafisha sekta hiyo inayokabiliwa na ufisadi wa hali ya juu.
Utajiri wa madini wa Congo Kinshasa umekuwa kichocheo kikuu cha mzozo wa miaka mingi nchini humo.
Eritrea yakanusha kusaidia kundi la Al Shabab.

Asmara, Eritrea -03/11/2011. Serikali ya Eritrea imekanusha ya kuwa inawasaidia kijeshi na kisiraha kundi la Al Shabab lililopo nchini Somalia.
Habari zilizo patikana kutoka serikali ya Kenya na Somalia zimesema " serikali ya Eritrea imetuma ndege yenye dhana za kijeshi kwa kundi la Al Shabab."
Hata hivyo serikali ya Eritrea ilisisitiza yakuwa habari hizo ni za uongo, hazina ukweli na hazina ushahidi."
"Na tumekuwa tukisema nguvu za kijeshi hazita leta amani nchini Somalia."
Somalia nchi ambayo ipo kwenye kona ya Afrika Mashari na imekuwa na vita vya wenye kwa wenyewe kwamuda usiopungua miaka 20.
Iran yaonya mpango wa kutaka kuishambulia kijeshi.

Tehran, Iran - 03/11/2011. Mkuu wa jeshi la Iran ameonya kitendo au jaribio la kuishambulia Iran, kitakuwa ni kitendo ambacho kitasababisha majuto makubwa.
Amir Ali Hajizadeh alisema " Iran inauwezo wa kutengeneza siraha na mizinga ya aina yoyote japo kunatishio kutoka nchi za Magharibi."
Na siraha hizo zinauwezo wa kwenda km 2,000 jambo ambalo hatuoni haja ya kufanya hivyo."
Mkuu huyo wa jeshi aliyasema hayo baada ya jeshi la Izrael kufanya majaribio ya mizinga yake yenye uwezo wa kufika hadi Iran.
Hadi sasa kuna habari zinasema "waziri mkuu wa Izrael Benyamin Netanyahu na washiriki wake wakuu wanajaribu kusisitiza nguvu za kijeshi zitumike zidi ya Iran ili kuharibu mitambo ya kinyuklia iliyopo humo."
Iran imekuwa ikishinikizwa nchi za Magharibi kusimamisha miradi yake ya kinyukli kwa madai ya kuwa Iran inampango wa kutengeneza siraha za kinyuklia, jambo ambalo Iran imekuwa ikilikana na kudai miradi yake ya kinyuklia ni kwa ajili ya kusaidia ukuzaji wa kisayansi.
Waziri mkuu wa Ugiriki akumbwa na wakati mgumu wa maamuzi.

Athense, Ugiriki - 03/11/2011. Waziri mkuu wa Ugiriki amekuwa na wakati mgumu kiuamuzi baada ya kutangaza yakuwa nchi yake haitapiga tena kura ya maoni kuhusu mkopo ambao nchi hiyo inauhitaji.
George Papandreou alisema "tumeanza kuzumngumza na vyama vipanzani ili kupata muafaka wa swala zima la kifedha tunazo hitaji."
Naomba tuungane katika swala hili ili kuikwamua nchi yetu kiuchumi."
Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya walishikwa na mshangao baada ya waziri mkuu wa Giriki kutangaza ya mkuwa ataitisha kura ya maoni ilikujua maoni ya wanchi juu ya mkopo unaotarajiwa kupewa nchi ya Giriki ili kujikwamua kiuchumi.
1 comment:
thanks 4 blog
http://bdallnewspaper.blogspot.com/
Post a Comment