Wednesday, July 15, 2009

Rais, Muammar Gaddafi,NAM, ipataiwe kiti cha kudumu cha Usalama UN.

Wairan na Walmania wakumbwa na msiba.

Qazvin, Iran - 15/07/09. Ndege ya shirika la ndege la Caspian imedondoka na kuuwa watu wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo.
Kwa muibu wa msemaji wa serikali wa Iran,Mohammed Reza Montezer Khorasan, alisema ndege hiyo ambayo ilikuwa imebeba watu wapatao 168 kutoka Iran Tehran na kuelekea jijini Yerevan Almenia, ilianguka karibu na mji wa Qazvin siku ya leo jumajatano, na kuwaauwa watu wote waliokuwemo kwenye ndege hiyo, wafanyakazi 15 na abiria 153.
Chanzo cha ajali bado kinachunguzwa, alimaliza msemaji huyo wa serikali.
Picha hapo juu, anaonekana, mmoja wa mama aliyepoteza ndugu zake katika ajali hii, akiwa analia kwa uchungu uku akisaidiwa na ndugu wengine.
Picha ya pili ni shirika la ndege la Caspiana Airline, ambapo moja ya ndege yake imeanguka na kupoteza maisha ya watu wapatao 168.
Picha ya tatu, wanaonekana wafanyakazi wa shirika la kutoa huduma ya kwanza wa Iran, wakiwa wamebeba baadhi ya mabaki ya miili ya watu waliopata ajali na ndege.
Picha ya mwisho, inaonekana,moja ya enjini ya ndege, ikiwa imeharibika vibaya ,ka kutupwa mbala na eneo ambalo ndege iliangukia.
Vita vya Gaza, habari tata za aanza kusikika hazarani?" Izrael".
Jerusalem,Izrael, - 15/07/09. Baada ya miezi sita kupita tangu, kusimama kwa vita kati ya kundi la Hamas na Izrael, baadhi ya wanajeshi wa Izrael, wamekuwa wakieleza matukio tofauti yaliyotokea wakati wa vita hivyo, ambavyo vilialibu vibaya eneo zima la Ukanda wa Gaza.
Wanajeshi hao, walisema ya kuwa matimizi ya siraha zenye gasi ya kunguza, zilitumika kwa nyakati fulani, na kudai kuna wakati mwingine waliamuliwa kuchukua hatua ambazo haziendani na maadili ya kijeshi.
Hata, hivyo , msemaji wa jeshi la Israel,Leutenant Colonel, Avital Leibovich, alikanusha madai hayo. na kusema madai hayo siya ukweli na hayana ushahidi wala tarehe ya matukio.
Picha hapo juu, ni ya moja ya tanki la kijeshi la Izrael likiwa mstari wa mbele katka maeneo ya Ukanda wa Gaza.
Rais,Muammar Gaddifi,NAM ipatiwe kiti cha kudumu cha usalama wa UN.
Sharm el Sheikh, Misri - 15/07/09. Rasi wa Libya, Muammar Gaddadfi, ameshutumu, Balaza la Usalama la Umoja wa mataifa ni kama chombo cha kutishia, ambacho kinatumika kwa baadhi ya nchi zenye viti vya kudumu katika kamati hiyo,na kunyima usawa katika maamuzi muhimu ya dunia, hasa kwa nchi masikini. aliyasema haya katika mkutano wa viongozi wa nchi zisizofungamana na upande wowote unaofanyika nchini Misri (Non Aligned Movement)
Akiongezea , rais Muammar Gaddafi, alisema wakati umefika wa NAM, kuwa na kiti katika kamati hiyo ya usalama ya umoja wa Mataifa , kwani tumekuwa tunajaziwa siraha na sasa zina kuwa mzigo kwa nchi wanachama wa NAM.
NAM, ambayo ni jumuia ya nchi zitokazo, Afrika, Asia na Latin Amerika.
Picha hapo, ni ya rais wa Libya, Moammar Gaddafi, ambaye amateaka NAM, ipatiwe kiti, katika balaza la Usalama la Umoja wa mataifa.
Kiongozi wa Al Qaeda namba mbili achomoza tena katika mitandao.
Islamabad/Pakistan - 15/07/09. Kiongozi namba mbili wa kundi la Al Qaeda's Ayman al Zawahiri, amewataka wafuasi wa kundi lake na wa Pakistani kupigana na Amerika na washirika wake waliopo nchini Pakistani, kwa kudai wamekuja kuwatawala na kuchukua nchi ya Pakistani.
Ujumbe huo wa Ayman al Zawahiri, uliwekwa kwenye mitandano siku ya jumanne wiki hii.
Hamasa hiyo kutoka kwa kiongozi wa Al Qaeda namba mbili, zimekuja wakati majeshi ya Pakistani, Amerika na washiriki wake, wakizidisha mashambulizi zidi ya kundi la Taliban na washiriki wake hivi karibuni katika eneo la maporomoko na mabonde ya Swat. Picha hapo juu ,ni ya Al Qaeda, Ayman al Zawahiri, akiongea kwa ujumbe wake katika moja ya mitandao ya kisasa.
Picha ya pili, wanaonekana, wanajeshi wa Pakistani, wakiwa katika doria, kulinda maeneo yao ili yasishambuliwe na Taliban na washiriki wake.

No comments: