Tuesday, July 21, 2009

Taliban watumia mbinu mpya katika kutengeneza nyenzo zao za kivita.

Swala la Rio Tinto, serikali mbili kukutana kuliongea.

Sydney, Australia - 22/07/09. Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Australia Stephen Smith, amesema atakutana na waziri wa mambo ya nchi za nje wa China Yang Jienchi,ili kuzungumzia mgogoro uliopo kati ya serikali hizi mbili, kufuatia China kumkamata mkubwa anayesimamia kampuni ya Rio Tinto, Stern Hu, ambaye ni rai wa Australia.
Stern Hu, alikamatwa July 5/2009 na serikali ya China, kwa madai ya upelelezi na kutaka kutoa rushwa kwa baadhi ya wafanyakazi ili aweze kuapata siri ya mikataba inavyotolewa .
China imekuwa ikifanya biashara na Australia,na hasa katika usambazaji wa vyuma, ambapo kampuni ya Rio Tinto, ndiyo kampuni mama katika uchimbaji na usambazaji.
Picha hapo, juu ni moja ya mitambo ya Rio Tinto, kampuni ambayo ni maarufu kwa uchimbaji wa madini kutoka ardhini.
Picha ya pili ni ya Stern Hu, ambaye kwa sasa yupo kizuizini nchini China kwa kudaiwa kuhusika na makosa ya jinai.
Nchini wanachama wa EU wapewa ruhusa kuweka akiba ya gas asilia.
Brussel, Ubeligiji - 22/07/09. Muungano wa Ulaya, umeziagizia nchi wanachama kuanza kuweka akiba ya gas ya asili, endapo kutatokea kutokuelewa tena na Urussi.
Kwa mujibu wa kamati inayo shughulikia maswala hayo imesema yakuwa kila nchi mwanachama, inatakiwa kuwa na gas ya asili ya kutosha ifikapo mwaka 2014, na gasi hiyo iwe na uwezo wa kutumika kwa muda wa miezi hadi miwili (Siku 60).
Mgogoro wa gas kutoka Urussi, umekuwa ukizisumbua nchi nyingi za Muungano wa Ulaya,kwa muda mrefu na kusababisha baadhi ya nchi kutiliana mkataba na Uturuki, ili kujengwa mabomba mapya yatakayo wezesha gas kutoka Caspian na Mashariki ya Kati,ili kupunguza kuitegemea Urussi katika upatikanaji wa gas.
Picha hapo juu,ni ya nembo ya nchi wanachama wa Muungano wa Ulaya, ambapo nchi wana chama wamekuwa wakipata msukosuko wa kupata gasi, pindipo panapotokea mtafaruki.
Picha ya pili ni moja ya mitambo ianayo tumika kuhifadhi gas, ambapo kuanzia sasa mitambo hiyo itabidi iongezewe uwezo wa kuhifadhi gasi hiyo.
Taliban, watumia mbinu mpya katika kutengeneza nyenzo zao za kivita.
Gardez ,Afghanistan - 22/07/09. Wapinaji wa kundi la taliban, wameshambulia maeneo ya yaliyopo majengo na ofisi za serikali kwenye miji tofatuini ncini Afghanistan.
Maeneo hayo ambayo yameshambuliwa yapo katika miji ya, Gardez na Jalalabad,wakati nchi hiyo inajiandaa mna uchaguzi wa rais utakao fanyika mwisho wa mwaka huu.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali, watu watun sita waliova nguo za kike, huku wakiwa na siraha na mabomu, walishambulia maeneo hayo tofauti ya serikali.
Kundi la Talibani limekuwa likitumia mbinu za kisasa kutengeneza mabobu yake, kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya kijeshi.
Hata hivyo , walinzi wa serikali waliweza kuwaua watu watatu, na wengine watatu waliweza kukumbia.
Picha hapo juu, wanaonekana, baadhi ya wanajeshi wakiimgia katika helkopta tayari kwenda mstari wa mbele kupambana na kundi la Talibani.
Picha ya pili, ni anaonekana mmoja ya mwanajeshi akikimbia, kukwepa bomu, ambalo lililipuka karibu yake.
Vijana wamiminika katika hospitali na zahanati kufanyiwa operesheni(Kutailiwa).
Bloemfontein, Afrika ya Kusini - 22/07/09.Kutokana na kuthibitishwa ya kuwa wanaume waliotailiwa wana nafasi kubwa ya kutoambukizwa ugonjwa wa ukimwi,vijana walio wengi nchini Afrika ya Kusini, wanamiminika katika zahanati tofauti ili kufanyikwa operesheni hiyo ndogo( Kutailiwa)
Kwa mujibu wa mmoja wa madokta ambao wanashughulikia operesheni hizo Dr, Diono Rech, alisema amekuwa anafanya operasheni hizo hadi kufikia 50 kwa wiki.
Picha hapo juu, wanaonekana, baadhi ya vijana wakiwa katika zahanati moja, tayari kufanyiwa opereshieni au ( Kutailiwa).
Kansa ya mapafu yajadiliwa kiundani na wataalamu jijini New York.
New York, Amerika - 22/07.09. Wanasayanchi nchini Amerika, wamesema ni hivi karibuni, walipo kutana jijini, New Yor, kwatafanikiwa vipi kutibu kansa ya mapafu,kwa kutumia vyombo ya kitaalamu zaidi.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana kutoka katika mahaabara inayo shughulikia uchunguzi na matibabu ya kansa, iliyopo jijini New York,zilisema muda si mrefu wataalamu wataamua ni njia ipi iliyo bora zaidi katika kutibu ugonjwa huo.
Picha hapo juu, ni ya mapafu, ambapo wataalamu wana sema muda si mrefu waataanza kutumia vidonge kuanza kutibu mapafu yaliyo kuwa na kansa.
Mamiliona washuhudia kupatwa kwa jua barani Asia.
Bangkok , Thailand - 22/07/07. watu wapatap millioni katika bara la Asia, wamekusanyika katika sehu maalumu zilizo tayarishwa kwaajili ya kuangalia kupatwa kwa jua katika karne hii.
Kwa mujibu wa wataalamu wa mambo ya kijiografia, wamesema ya kuwa, maeneo tofauti katika bara la Asia, Japan, India ,na China,wataweza kuona kitend hicho ambacho hutokea kwa mara moja katika kila bara
Picha hapo juu, ni ya jua linaonekana kuzibwa kabisa , na kuleta giza kwa muda katika eneo ambalo lilitakiwa jua liwe linawaka.
Picha pili hapo juu wanaonekana, baadhi ya wanafunzi, wa wanaosomea maswala ya sayansi, wakiangali kupatwa kwa jua katika jimbo la Bihar nchini India.

No comments: