Tuesday, July 28, 2009

China na Amerika zakutana kujadili ushirikiano wa kiuchumi.

Unene wa mwili ni hali ya hatari kwa mtu na matumizi ya serikali.

Chicago, Amerika - 28/07/09. Swala la kunenepa kwa watu kupita kiasi hasa katika nchi za Magharibi, zimekuwa zinaleta vichwa kuuma kwa watu na jamii nzima ya maeneo haya.
Kwa mujibu wa wachunguzi wa wa mambo ya afya ya watu, zinasema ya kuwa unene wa mwili ni hali ya hatari kwa binadamu mwenyewe na serikali za nchi hizo kwa kutumia pesa nyingi katika matibabu yanayo sababishwa na unene wa mwili.
Akiongea haya, Dr Thomas Frieden, alisema hipo haja ya watu kwa kusaidiana na serikali kupambana na hali hii.
Picha hapo juu, anaonekana mmoja ya watu, ambao unene umekuwa ukiwa tatizo kwa jamii.
Picha ya pili, wanaonekana, baadhi ya watu wa nchi za Magharibi, ambao wanakabiliwa na hali ya kuongezeka kwa watu kuwa wanene kupita kiasi, na kutetetlesha hali ya afya zao.
Utumiaji wa simu ya mikono huku ukiendesha gari, ni hatari kwa watumiaji wa barabara.
Virginia, Amerika - 28/07/09. Wataalamu wa mambo ya usalama barabarani, wamesema yakuwa kuna ya asilimia kubwa kwa dereva anaye endesha gari wakati anaandika teksti kwa kutumia simu ya mkono kupata ajali, au kusababisha ajali kwa madereva wengine wanaotumia barabara wakati huo.
Kwa mujibu wa wataalamu kutoka chuo cha usafiri cha Virginia, zimesema kugonga ao kugongana na gari jingine kuanaweza kutokea wakati wowote wakati dereva anaandika teksti kwa kutumua simu ya mkono huku akiwa anaendesha gari.
Wachunguzi hao walisema, hata upokeaji wa simu kwa kutumia mkono kuhu uanendesha gari, kunaleta hatari pia.
Picha hapo juu, ni moja ya picha za video zinaonyesha kwa kiasi gani dereva, anapo endesha gari, huku huku akituma teksti anaweza sababisha ajali barabarani.
China na Amerika zakutana kujadili ushirikiano wa kiuchumi.
Washington,Amerika - 28/07/09. Rais wa Amerika, Baraka Obama, ameukaribisha uhusiano wa Amerika na China na kutaka uwe wa faida kwa nchini zote mbili na wanachi wake.
Rais , Obama aliyaongea hayo wakati alipo kuwa anawakaribisha viongozi wa China wakiongozwa na makamu wa waziri mkuu wa China, Wang Quishan.
Ujumbe huo kutoka China, upo nchini Amerika, kujadili ni jinsi gani nchi hizi mbili zitashirikiana kiuchumi.
Picha hapo juu, anaonekana rais, Obama, akiongea mbele ya wajumbe wa China na Amerika kabla ya kuanza mjadiliano ya kiuchumi.
Picha ya pili,rais , Baraka Obama, akimkaribisha, makamu wa waziri mkuu wa China, Wang Qishan, na kulia ni waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, Bi Hillary Clinton.
Picha ya tatu, wanaonekana wajumbe na viongozi kutoka China,wakimsikiliza rais wa Amerika, Baraka Obama wakati wa ufunguzi wa mazungumzo ya kiuchumi wa nchi hizo mbili, (Amerika na China)
Sijawahi kula nyama ya mtu, adai rais wa zamani wa Liberia.
Hague,Nederland - 28/07/09. Rais wa zamani wa Liberia , Charles Taylor, amekanu sha shutuma zakuwa alikuwa anatafuta na kula nyama za watu, na kuesam nu upuuzi mtupu.
Akiongea kwa msisitizo , rais huyo wa zamani wa Liberia, Charles Talor, aliambia koti ya kuwa watakuwa ni wagonjwa kama wakiamini ushaidi unaotolewa juu yake yakuwa alikuwa ana kula nyama za watu, inafanya mtu aweze kutapika.
Rais huyo wa zamani wa Liberia, anakabiliwa na makosa ya kukiuka haki za binandamu,na ya kivita zidi ya nchi ya Sierra Leone.
Picha hpo juu anaonekana, rais wa zamani wa Liberia , Charles Taylor, akiwa mahakani, huku akiandika pointi na huku akisikiliza shutuma zidi yake.
Machafuko yaleta hali ya wasiwasi nchini Nigeria.
Kano , Nigeria - 28/07/09. Hali ya usalama nchini Nigeria imeingia katika hali ya utata, hasa katika eneo la jimbo la Kano, lililopo kaskazini mwa Nigeria.
Kufuatia machafuko hayo amboyo bado yanaendelea chini humo katika jimbo la Kano,yamesababisha baadhi ya watu kupoteza maisha yao.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema watu wapatao 100, wamesha poteza maisha mpaka sasa.
Ghasia hizo ambazo zinakuja baada ya wakazi wa eneo hilo la Kano, hawakubaliani na mpango wa elimu ya kisasa, kwa madai yakuwa haiendani na matakwa ya jamii hii, na wanataka elimu iwe inaendana na dini yao ya Uislaam.
Kufuatia mvutano huo, watu walikwenda kuvamia kituo cha polisi,kwa madai ya kuwa kuna mmoja ya mwenzao amekamatwa, na hivyo polisi kujibu mashambulizi na kuteta maafa makubwa.
Picha hapo juu, wanaonekana baadhi ya watu wakiwa chini ya ulinzi, mara baada ya kutiwa chini ya ulinzi.

No comments: