Tuesday, July 14, 2009

Rais wa zamani wa Liberia akanusha mashitaka zidi yake.

Muungano wa Ulaya wapata rais mpya. Brussels, Ubeligiji - 14/07/09.Mbuge wa Poland, Jerzy Buzek, amechaguliwa kuwa rais wa bunge la muungano wa Ulaya, baada ya kuchaguliwa kwa kura nyingi zaid ya 555 kati ya kura 644 zilizo pigwa katika uchaguzi wa rais wa bunge la muungano wa Ulaya. Mbunge, Jerzy Buzek, ambaye ni mbuge wa mlango wa kati kimsimamo, amechaguliwa, ikiwa nchi yake ina miaka minne tangu kujiunga na muungano wa Ulaya. Picha hapo juu, anaonekana, rais wa sasa wa muungano wa Ulaya, akiongea mara baada ya kuchaguliwa kwake.

Rais wa Liberia atuhumiwa na kwa kuhusika kusaidia vita.
Monrovia ,Liberia - 14/07/09. Rais wa sasa wa Liberia,Ellen - Sirleaf, amekumbwa na wakati mgumu, baada ya kamati inayo simamia hali halisi ya uharibifu wa vita nchini Liberia, umeomba rais wa Liberia asimamishwe uongozi wake kwa kuhusika na kundi moja ambalo, lilikuwa likipigana miaka 20 iliyo pita nchini Liberia.
Kamati,inayo shughulika mapatana, mariziano na kusameheana,inasema yakuwa katika watu ambao wametajwa ni rais wa sasa wa Liberia, Ellen - Sirleaf, kwa kuhusika kwa karibu na uongozi wa rais wa zamani Charles Tayrol, ambaye yupo Hague, kujibu mashitaka yana yo mkabili zidi yake.
Hata hivyo, msemaji wa rais , Ellen Serleaf, Cyrus Badio, amesema yakuwa rais ,bado anatafakali ripoti hiyo na ataongea hapo baadaye.
Rais wa zamani wa Liberia, akanusha mashitaka zidi yake.

Hague, Holland - 14/07/09. Rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor ametoa ushahidi wake leo zidi ya makosa 11, ambayo yanamkabili.

Akiongea, mbele ya jaji, rais huyo wa zamani wa Liberia,Charles Taylor,alisema ya kuwa makosa zidi yake ni ya , uzushi,uongo ulio jaa fununu za ajabu,uvumi, na hayana ukweli ndani yake na wale wanao zania ya kuwa yeye alihusika,katika mauaji na machafuko ya liyotokea nchini Sierra Leone.

Machafuko na mauaji hayo yaliyo tokea mwaka 1991 - 2001, yalipoteza maisha ya watu wapatao 200,000. Hata hivyo kesi hii bado inaendelea. Picha hapo juu, anaonekana, rais wa zamani wa Liberia Charles Tayrol kushoto, akiwa mahakamani kutoa ushahidi wake.

No comments: