Thursday, July 2, 2009

Binti aliyepona katika ajali ya ndege akutana na baba yake.

Historia na ndoto za Williams za jirudia nchini Uingereza. Wimbledon, Uingereza - 02/07/09. Historia ya mchezo wa tenisi, imejirudia tena, baada ya ndugu wawili mkubwa na mdogo,kukutana tena katika fainali ya kugombea kikombe cha Wimbledon. Ndugu hao , mabao pia ni Dada mdogo Serena Williams na dada mkubwa Venus Williams, watakutana mara ya kibarua kigumu cha kupambana na kushinda michezo yote ya tenisi kwa upande wa wanawake, kutoka hatua ya mwanzo hadi kufikia kukutana fainali. Katika, mchezo wa nusu fainali, Serena aliweza kumshinda, Elena Demetieva kwa seti 7-5,8-6, japo kayika seti ya kwanza Serena alishindwa kwa seti 6-7. Naye dada Venus, alishinda , bila huruma Dinara Safina kwa seti 6-1,6-0. Kufuatia ushindi wa madada hawa, Venus na Serena , ambao wanazaliwa na mama na baba mmoja, kumewafanya wakutane tena katika fainali ya Wimbledon kwa mara ya nne. Kukutana kwa madada hao,kunazidi dhihirisha ya kuwa ndoto zao walizo kuwa wakiziota miaka 20 iliyo pita kwenye mji walio kulia, Compton Califonia za kukutana kwenye fainali ya mashindano makubwa inakuja kila wanapo amua kufanya kazi ya ziada, alisema Venus. Picha hapo juu wanaonekana, madada mgogo Serena Williams kulia na mkubwa Venus Williams, wakiwa wameshikilia vikombe vya ubingwa wa tenisi kwa upande wa wanawake, baada ya kushinda (DOUBLES) wawili kwa wawili hapo miaka ya nyuma nchi Uingereza. Korea ya Kaskazini, yazidi kutunisha misuri kwa jumuia ya Kimataifa. Pyongyang, Korea ya Kaskazini - 02/07/09.Kora ya Kusini, imerusha makomora ya masafa mafupi hivi karibuni. Kwa mijibu wa Yanhap, shirika la utangazaji, limesema, makombora hayo yalirushwa kuelekea upande wa mashariki ya pwani. Makombora ambayo yallirushwa nia nchi kavu , hewani kuelekea kwenye melikebu. Makombora hayo yanajulikana kama, Silkwom. Kurushwa kwa makombora hayo, kumeweka hali ya wasiwasi katika eneo zima, hasa kati ya Korea ya Kusini na Korea ya Kaskazini. Picha hapo juu, nia moja ya michongo ya makombora yakiwa yamewekwa kama minara kwenye sehemu moja ya mji, nchini Korea ya Kaskazini. Binti aliyepona katika ajali ya ndege, akutana na baba yake.

Paris, Ufaransa - 02/07/09. Baba ya msichana aliyepona katiaka ajaili ya ndege ya shirka la Yemen,amempokea binti yake, Bahia Bakari, wakati alipo wasili nchini Ufaransa baada ya kupata matibabu ya kwanza nchini Komoro.
Binti huyu, Bahia Bakari, ndiye abiria pekee, aliye jaliwa kuwa hai katika jali hiyo.
Ndege aina ya Airbus, ilianguka siku ya jumanne alfhajiri katika bahari ya Indi wakati ikitokea, Sanaa Yemen kuelekea visiwa vya Komoro.
Picha, hapo juu wanaoneka,Kassim Bakari, babaya Bahia Bakari, akiwa ameshikilia, binti yake, huku wakiwa njiani kuelekea hospital, mapema alipo wasili Paris.
Picha ya pili ni ya shrika la ndege la Yemen,ambapo moja ya ndege yake, ilianguka siku ya jumanne alfhajiri.
Umoja wa mataifa wapata mkurugenzi mkuu mpya wa kusimamia atomi na nyuklia.
Viena , Austria - 02/07/09. Shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ukaguzi wa nguvu za atomi na nyuklia ( International Atomic Enegy Agency), limemchagua Yukiya Amano kuwa mkurugenzi wake mkuu, ili kushika nafasi itakayo achwa wazi na mkurugenzi wa sasa, Mohamed El Baradei kuanzia mwezi November 2009.
Katika uchaguzi, huo,Yukiya Amano, alimshinda mpinzani wake mkuu, Abdul Samad Minty, kutokea Afrika ya Kusini kwa kupata kura 35,kutoka kwa nchi wanchama.
Picha hapo juu, anaoneka Yukiya Amano,ambaye atashikia kiti cha ukurugenzi mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ukaguzi wa nguvu za atomi na nyuklia,kuanzia mwezi wa November 2009.
Picha ya pili, wanaonekana, kushoto mkurugenzi mkuu wa sasa,Mohamed El baradei, akiwa na mkurugenzi mchaguliwa Yukiya Amano, wakati walipo pokea zawadi ya nishani ya Nobel nchini Norway mwaka 2005.

No comments: