Sunday, July 5, 2009

Serena na Venus Williams Malkia wa tenis wa Wimbledon 2009.

Serena na Venus Williams, Malkia wa tenis wa Wimbledon 2009.

Wimbledon, Uingereza 05/07/09. Kwa mara nyingine tena, Serena na dada yake Venus, wameweza kushinda mchezo wa tenis kwa wanawake na kuchukua kikombe cha Wimbledon kwa ushindi wa seti 7-6, 6-4 zidi ya Samantha Stosur na Rennae Stubbs.
Huku wakiwa na furuha, Venus alisema ya kuwa ushindi huu umekuja kutokana na jitihada yao, na kwa kuzingatia tumecheza zaidi ya masaa matatu jana na leo,hivyo inabidi tuwe na furaha kwa kutokubali kuruhusi uchovyo ututalawale.
Senena, ambaye alishinda siku ya jumamosi kwa upande wa wanawake, alisema huwa anajisikia furaha saana anaposhinda huku akiwa na dada yake pamoja katika mchezo wa wawili wawili.
Picha hapo juu wanaonekana , Serena na Venus Williams, wakiwa wamechikia vikombe vya ushindi baada ya kushinda tenis fainali wanawake katika mchezo wa wawili wawili.
Picha ya pili, wanaoneka Venus kulia akienda kumkumbatia mdogo wake Serena, mara ya kushinda seti ya mwisho iliyo wapa ubingwa.
Picha ya tatu, anaonekana , Serena akiangalia kwa tabasamu sahani ya ubingwa wa tenis wa Wimbledon,mara baada ya kukabidhiwa.
Picha ya nne, anaonekanam Serena , akilionyesha sahani la ubingwa wa tenis, kwa upande wa wanawake, baada ya kushinda dada yake Venus.
Picha ya tano, anaonekana, Venus hali siyo nzuri, wakati alipo kuwa akishindana na mdogo wake kugombania ubingwa wa kombe la teni wanawake la Wimbledon.
Picha ya sita, wanaonekana, Serena akimkubatia dada yake, Venus , mara baada ya mpambano kati yao, ambao Serena aliweza kumshinda dada yake.
Picha ya saba, anaonekana, Serena , akiwa amepiga magoto kushangilia, ushindi zidi ya dada yake.
Roger Federer,aweka rekodi ya mchezo wa tenis duniani.
Wimbledon Uingereza - 05/06/07.Roger Federer, ameshinda kombe la Wimbledon katika mchezo wa tenis , na kuweka rekodi ya kuwa ushindi wa mashindano makubwa ya tenis kwa mara ya 15.
Katika pambano hili ambalo lilimpa Roger Ushindi zidi ya Andy Rodick, kwa kumshinda kwa seti 5-7 (6) ,7-6,(5), 3-6 na 16-14.
Roger Federer, ambaye ameshinda fainali za Wimbledon mara 6,katika mchezo uliowachukua muda wa masaa 4 : 18dk.
Picha hapo juu anaonekna Roger Federer, akiuchonga mpira ambao ulimshinda, Andy Rodick, na kumpa ushindi, Roger Federer kwa seti 16-14.
Picha ya pili, anaonekna Roger Fedrer, akiwasalimia kwa furuaha wapenzi wa mchezo wa tenis waliokuja kushuhudia pambano kali kati yake na Andy Rodick.
Picha ya tatu, anaonekana, Roger Fedrer, akibusu kikombe cha ubingwa cha mchezo wa tenis, mara baada ya kukabiziwa kikombe hicho.
Amerika na Urussi kuziba ufa uliopo?
Moscow Urussi -05/07/09. Rais wa Urussi, Dimirti Medvedev, atakuwa mwemyeji wa rais wa Amerika, Baraka Obama hivi karibuni, ili kuzidi kuimarisha uhusiano wa karibu.
Ziara ya rais Baraka Obama nchini Urussi, itakuwa ni pili katika bara la Ulaya, baada ya mkutano wa kiuchumi ulifanyika mjini London Uingereza.
Mambo mengine yatakyo zungumziwa ni maswala ya makombora ya kivita ambayo Amerika inampango wa kuyakeka katika moja ya nchi moja ya Ulaya, jambo ambalo Urussi inalipinga vikali.
Picha ya hapo juu wanaonekana, raia wa Urussi, Dimitri Medvedev, akiwa anamnongoneza waziri mkuu wa Urussi, Vladamir Putin.
AU haihukubaliana na mahakama ya kimataifa. rais, Al - Bashir yupo huru kusafiri.
Tripol Libya - 04/07/09. Kikao cha viongozi wa Afrika kimamua kwa pamoja ya kuwa nchi za Afrika hazita husika katika kumkamata au kumkamata rais wa Sudan, Omar Al - Bashir.
Uamuzi huo ulichukuliwa na wakati viongozi wa muungano wa nchi za Afrika walipo kutana chini ya uwenyekiti wa rais wa Libya Muhamar Ghadafffi.
Rasi wa Sudan, anakabiliwa na kesi ambayo imefunguliwa zidi yake na mahakama inayo shughulikia kesi za ukiukaji wa haki za binadamu iliyopo nchi Nederland (The Hague).
Kufuatia uamuzi huo, rais wa Sudan anaweza safiri katika nchi yoyote ya Afrika bila kuwa na wasiwasi, kwa kuzingatia nchi 33 za Afrika zilikubaliana na kutia sahii makubaliano ya mjini Rome Itali,ya kufungua mahakama itakayo shughulikia kesi za ukiukwaji wa haki za binadamu iliyopo nchi Nederland.
Picha hapo juu, anaonekna rais , wa Sudan, Omar Al bashir , akiwa katika kikao cha viongozi wa Afrika kilicho fanyika hivi karibuni.

1 comment:

Célio said...

Ola...
Passando para uma visitinha em seu blog. Muito interessante, parabéns.
Abraços.