Tuesday, November 30, 2010

Mkutano wa utunzaji wa mazingira waanza kwa mashaka.

Google kufanyiwa uchunguzi na jumuia ya Ulaya. Brussel, Umoja wa Ulaya - 30/11/2010. Kitengo cha uchunguzi cha jumuia ya muungano wa umoja wa Ulaya kinachunguza malalamiko yaliyo tolewa dhidi ya Google kwa kukutumia vibaya umezo wake. Kwa mujibu wa makampuni mengine ya kimtando yamsema "google inavunja ushindani wa kiimtandao dhidi ya makampuni washindani." PIcha hapo juu inaonekana picha ya mtandao wa Google ambao unalalamikiwa na washindani wake kwa kuvunja ushindani. Mkutano wa kutunza mazingira waanza kwa mashaka. Cancun,Mexico - 30/11/2010. Mkutano wa kutunza mazingira unaofanyika nchini Mexico umeamza kwa vishindo huku kila nchi muhusika akitaka matakwa yake yatimizwe. Akiongea katika mkutano huo mwakilishi wa serikali ya Amerik Jonathan Pershinga alisema " tunataka kuwepo na makubaliano ya pamoja katika kudhibiti uaribifu wa mazingira duniani" Hata hivyo msimamo huo wa Amerika umeonekana kutiliwa mashaka na baadhi ya washiriki kwa kudai kuwa hakutaleta matokeo mazuri. Pichani hapo juu aanonekana mmoja ya washiriki wa mkutano wa mazingira unaofanyika Mexico akichora kapicha kuashiria ishara kuhusu matokeo ya mikutano iliyo fanyika hapo awali kabla wa sasa unaofanyika Cancun Mexico ambapo wajumbe wa nchi tofauti wanakutana kujadili mazingira. Venezuela yapewa mkopo na Urussi kwa ajili ya kuimarisha maswala ya kiulinzi. Carakas, Venezuela 30/11/2010. Serikali ya Venezuela imesema ya kuwa serikali ya Urussi itaipa mkopo wa $4 billion ambazo zitaiwezesha nchi hiyo kukuawa siraha ili kuimarisha maswala ya kijeshi na ulinzi. Akiongea katika sherehe ya miaka 90 ya jeshi la anga rais wa Venezuela Hugo Chavez alisema " Tumeamua kufanya hivyo ili kuendelea kulinda nchi yetu na maadui." Picha hapo anaonekana rais wa Venezuela Hugo Chavez wakati wa kuadhimisha sherehe za maiaka 90 ya jeshi la anga ambalo ilitaongezewa nguvu. Radi yaleta maafa na vifo ya watu nchi Afrika ya Kusini. Kwa Zulu Natali, Afrika ya Kusini - 30/11/2010.Watu wapatao saba na wengine kujeruhiwa baada ya radi kuwashambulia wakati wakiangali jengo lilijenge kwa turubai kwaajili ya Krismas. Kwa mujibu wa msemaji wa serikali anayeshughulikia maafa Mthokozisi Duza alisema "watu walio jeruhiwa apo hospitali kwa matibabu." Picha hapo juu inaonyesha miali ya moto iliyo tokana na radi ikishambulia Kwa zulu Natal na kusababisha maafa ya kijamii na kwa mazingira. Rais wa Urussi atoa onyo ikiwa hakuna makubaliano na NATO.

Moscow, Urussi - 30/11/2010. Rais wa Urussi Dimtri Medvedev amesema ikiwa nchi yake aitafikiana makubaliano na NATO katika swala la kujenga mitambo ya kiulinzi basi nchi yake itajihami zaidi kiulinzi. Akilihutubuua taifa, rais Medvedev alisema "swali lililopo ni kwa NATO kukubaliana nasi katika swala zima la ujenzi wa mitambo ya ulinzi au ikiwa hakuna makubaliano basi katika kipindi cha miongo ijayao basi tutaamua kuweka mitambo yetu wenyewe ya kiulinzi na kufufua mashindano ya kisiraha." Pia rais Medvedev, aliwataka wanachi kuongeza kizazi kwa katika kipindi cha miaka ijayo taifa litakuwa na watu wachache na haitakuwa vizuri kwa ujenzi wa taifa." Picha hpo juu anaonekana rais wa Urusi Dimri Medvedev akihutubia taifa na kuongelea maswala ya kitaifa na kimataifa kwa ujumla. China inamatumaini ya kuwa ipo siku kutakuwa na Korea moja.
Beijing China 30/11/2010. Habari zilizo patikana kutoka kwa mtandao wa Wiki Leaks zinasema ya kuwa baadhi ya viongozi wa serikali ya China wanapendelea kuunga mkono na kuungana kwa Korea ya Kusini na ya Kaskazini.
Kwa mujibu wa habari zilizo patikana zinasema "balozi wa China nchini Kazakhstan alisema wanamatumaini siku za mbaleni kutakuwa na Korea moja ingawa kwa sasa bado nchi hizo zinajulikana kama zilivyo Korea ya Kusini na Korea ya Kaskazini."
Picha hapo juu ni bendera ya Korea ya Kaskazini nchi ambayo imekuwa ina vutana na jumuia ya Kimataifa kuhusu ukweli wa swala la kinyuklia na mshiriki wa karibu wa China.
Picha ya pili ni ya bendera ya Kora ya Kusini nchi ambayo imekuwa haina ushirikiano mzuri na serikali ya Korea ya Kaskazini.

1 comment:

Anonymous said...

We Mjamaa mbona sikuelewiii...?1 Hii blog yako ni ya habari za Kimataifa nini?

Yani Mwanzo mwisho habari za nyumbani hakuna.

Waiiiiiiiiii.
Siji tena.