Thursday, December 2, 2010

Kombe la dunia mwenyeji ni Urussi 2018 na Katar 2022.

Kombe la Dunia wenyeji ni Urussi 2018 na Katar 2022.

Zuriki,Swizland-02/12/2010. Shirkisho la soka duniani limepiga kura na kuchagua nchi ambazo zita kuwa wenyeji wa fainali ya mchezo wa soka wa mwaka 2018 na 2022.
Akitangaza wenyeji wa fainali wa soka hizo ambazo ni Urusi 2010 na Katar 2022.
Wakiongea kwa wakati tofauti viongozi wa kampeni wa za kutaka nchi zao kuwa wenyeji wa soka
" Tunawahakikishia mtafurahi na kuondoka na kumbukumbu za furaha" naye kiongozi wa Katar alisema " nawashukuru kwa kutupatia wananchi wa Katar uaminifu wenu na yote tuliyo haidi yatakamilishwa na kila atakaye hudhulia 2022 fasinali za soka, basi atomndoka na kumbukumbu ambazo zitakuwa na milele."
Picha ya hapo juu ni ya bendera ya Urussi nchi ambayo imechaguliwa kuwa mwenyeji wa kombe la fainali za soka mwaka 2022.
Picha ya pili anaonekana kiongozi wa kampeni ya kutaka kombe la dunia lichezwe nchini mwaka akilinyanyua kombe la dunia mara baada ya nchi yake kutangazwa kuwa mwnyeji wa kombe la dunia 2022 na kushoto ni rais wa FIFA Sepp Blatter.
Picha ya tatu ni ya bendera ya Katar nchi ya kwanza ya kiarabu kuandaa kombe la dunia.
Picha ya nne wanaonekana baadi ya wajumbe wa Katar wakipokea kombe la dunia kama ishara ya kukubaliwa kuwa mwenyeji wa mchezo wa soka 2022 mara baada ya Katar kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa fainal hiyo.
Mahakama ya kataa rufaa ya mwanzilishi wa WIKI leaks.
Stockholm, Sweden-02/12/2010.Mahakama kuu nchini Sweden imekataa rufaa ya mwanzilishi wa mtandao WIKI leaks ambaye anakabiliwa ya ubakaji.
Kwa mujibu wa msemaji wa mahakama Kerstin Norman alisema " mahakama imeamua kukataa rufani ya Julian Assange."
Julian Assange mwanzilishi wa WIKI Leaks mtandao ambao umetoa habari nyingi za kushutusha na hasa zile za nyaraka za siri za serikali tofauti.
Picha hapo juu anaoeneka Julian Assange, ambaye rufani yake imekataliwa akiongea na waandishi wa habari kuhusu hali halisi ya mtandao wake.
Picha ya pili ni nembo ya mtandao wa WIKI leaks ambao umehusika katika kutoa habari za nyaraka za siri.
Kampuni ya ndege ya Qantas yafungua kesi dhidi Rolls-Royce.
Sydney,Australia-02/12/2010. Kampuni inayohusika katika matengenezo ya injini za ndege ambazo zimekuwa zikileta matatizo na kusababisha baadhi ya injini za ndege kufanyiwa uchunguzi.
Kampuni hiyo Rolls-Royce ambayo ndiyo mtengenezaji wa injini hizo imetakiwa kulipa fidia kutokana na usumbufu uliofanywa na injini zake kwa kampuni ya ndege ya Qantas.
Hata hivyo kampuni ya Rolls-Royce imesema huwa inafanya uchunguzi wa hali ya juu katika injini zake kila wakati.
Picha hapo juu inaonekana moja ya injini ya shirika la ndege la Qantas ikiwa imeharibika vibaya mara baada ya kushika moto.
Rais wa Sri Lanka ashutumiwa kwa kuhusika na mauaji dhidi ya TAMIL Tigers.
London, Uingereza - 02/12/2010. Rais wa Sri Lanka ambaye yupo ziarani nchini Uingereza ametajwa ya kuwa anahusika kwa kiasi kikubwa katika mauaji yaliotokea wakati wa vita zidi ya kundi ta TAMIL Tigers.
Habari hizi ambazo ni moja ya mlolongo wa habari ambazo zimetolewa na mtandao wa WIKI Leaks zina eleza ya kuwa "rais wa Mahinda Rajapaska na washiriki wake wanahusika katika mauji wakati wa vita vyawenyewe kwa wenyewe (Kati ya serikali iliyopo madarakani na kundi la TAMIL Tigers ambalo linapingana na serikali."
Hata hivyo wapinzani wa Mahinda Rajapaska na serikali yake waliweza kuzuia kuendelea na mpango wa rais huyo kuhutubia katika mkutano uliopangwa ambapo kwa sasa yupo ziarani nchini UIngereza.

No comments: