Friday, December 3, 2010

Baraka Obama afanya ziara ya ghafla nchini Afghanistan.

Baraka Obama afanya ziara ya ghafla nchini Afghanistan. Kabul, Afghanistan - 03/12/2010. Rais wa Amerika amefanya ziara ya ghafla nchini Afghanistan na kuongea na wanajeshi na raia wa Amerika wanaoshiriki kwa katika vita zidi ya Taliban na washirkia wake. Akiongea katika hotuba hiyo rais Baraka Obama alisema "Amerika itaendelea na kupambana na wale wote ambao wanapinga maendeleo ya Amerika au kutishia usalama wa Amerika na watu wake, na hatutashindwa kamwe kuwasaka popote walipo." Hata hivyo katika ziara hiyo rais Baraka Obama, hakuweza kukutana na rais wa Afghanistan kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya. Picha hapo anaonekana rais wa Amerika Baraka Obama akishuka kutoka kwenye ndenge mara baada ya kuwasili nchini Afghanistan kwa mara ya pili akiwa kama rais wa Amerika ili kuwapa salamu za sikuku wanajeshi na kuelezea ni kwa jinsi gani Waamerika wote wapo pamoja nao. Ulaya ya kumbwa na mporomoko wa barafu. London, Uingereza - 03/12/2011. Bara la Ulaya limekumbwa na mporomoko wa barafu ambao umesababisha hali ya utoaji wa huduma kuyumba. Barafu hizo ambazo zinaendelea kugubika karibuni Ulaya kote tokea Urussi hadi Spain limekuwa gumzo kwa wakazi wengi wa eneo hili. Siku ya Jumanne barafu nyingi ilipolomoka na kusababisha hali ya hewa kuwa barisi hadi kufikia kati ya hasi 20 na 22. Picha hapo juu linaonekana moja ya gari la kusafisha njia likijaribu kutoa barafu ili huduma ziweze kuendelea zilishindikana kutokana na wingi wa barafu iliyo poromoka toka angani

No comments: